Wednesday, December 7, 2016

SERIKALI KUANZISHA TUZO KWA WAANDISHI WA BLOGS

k1
Na Beatrice Lyimo-MAELEZO
SERIKALI inatarajia kuanzisha tuzo za umahiri kwa waandishi wa habari wa mitandao ya kijamii (blogs) nchini kuanzia mwaka 2017.
Hayo yamesemwa leo jijini Dar  es salaam na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye wakati akifunga Mkutano Mkuu wa Tanzania Bloggers Network (TBN) na semina ya wanachama wa umoja wa waendeshaji wa blog nchini.
Waziri Nape alisema kuwa lengo la tuzo hizo ni kuzisaidia blogs za Tanzania kubobea katika nyanja tofauti ikiwemo kilimo, mifugo, viwanda, hifadhi ya jamii kwa nia ya kuipa heshima tasnia ya habari nchini.
Aidha, Waziri Nape alisema kuwa tayari Serikali imeanza mazungumzo na   makampuni na taasisi mbalimbali kwa ajili ya kudhamini tuzo hizo ili kuhakikisha kuwa washindi wanapatikana kwa uwazi.
“Tuzo hizo zitakuwa za kwanza kwa namna zitakavyoendeshwa kwa uwazi hivyo makampuni zaidi yanakaribishwa kuweza kudhamini mashindano hayo yatakayojielekeza kwenye nyanja tofauti” alisema Waziri Nape.
Waziri Nape pia alisema amewataka wamiliki na watendaji wa blogs nchini kushirikiana na Serikali ili kuweza kuijenga nchi.
“Tutumie fursa za kisiasa zilizopo, fursa za teknolojia ili kuhakikisha tiunajenga Tanzania tunayoitaka, ishaurini Serikali kwa kutumia taaluma mliyonayo ili kuweza kuipeleka nchi ya Tanzania tunayoitaka” alifafanua Waziri Nape.(P.T)

Tuesday, November 1, 2016

PICHA: WORLD VISION YAKABIDHI VIFAA VYA KUJIFUNGULIA KWA ZAHANATI TANO WILAYANI LONGIDO

Shirika la World Vision kupitia Mradi wake wa Maendeleo ya jamii Ketumbeine, umetoa msaada wa Vifaa vya Hosipitali vitakavyosaidia katika kurahisisha shughuli za Uzazi katika Zahanati tano zote zilizopo katika tarafa ya Ketumbeine wilayani Longido Mkoani Arusha.
Akizungumza katika Makabidhiano ya vifaa hivyo, Mwezeshaji wa Mradi huo Ndugu Elisante William amesema kuwa lengo la kutoa vifaa hivyo ni ili kupunguza tatizo la wanawake wanaojifungulia Majumbani ambapo muda mwingine inapelekea vifo vya wanawake wengi wajawazito pamoja na watoto.
"Shirika letu la kijamii kupitia mradi wake wa maendeleo Ketumbeine AP, tunayo furaha kukabidhi  kwa jamii ya Ketumbeine vifaa  vya Hospitali vitakavyo kabidhiwa katika Zahanati tano ambazo ni Noondoto, Losirwa, Lang’atadapash, Ilerienito, na Gilai Merugoi ambapo ni imani yetu kuwa vifaa hivi vitasaidia  kwa asilimia kubwa kupunguza tatizo la vifo kwa wanawake wajawazito vinavyosababishwa na kujifungulia Majumbani kutokana na ukosefu wa vifaa stahili katika zahanati" Alisema Elisante.
"Kwa takwimu za haraka haraka inaonyesha kuwa katika jamii hii kati ya wanawake mia wanaojifungua ni wanawakewatano tu ndo wanajifungulia hosipitali na hii nikutokana na umbali wa vituo vya afya vyenye vifaa vya kujifungulia," Aliongeza.
Akipokea Msaada huo Kwaniaba ya Mkurugenzi wa wilaya ya Longido Ndg Atuganile amesema kuwa wanapongeza shirika la World Vision kwa kuona changamoto katika sekta ya Afya iliyopo wilayani 

Bw Elisante William wapili kutoka kulia ambaye nimwezeshaji wa Mradi wa Afya  akikabidhi seti ya vifaa vya kujifungulia(Delivery Kit) pamoja na Vitanda vya kujifungulia(Delivery Beds) kwa  Bibi Atuganile  Chisunga anayepokea kwaniaba ya Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Longido.
Bibi Atuganile akitoa neno la Shukrani baada yakupokea Msaada huo.
 

SERIKALI YAANZA KUKAGUA NA KUHAKIKI VYETI VYA NDOA KWA WATUMISHI WA UMMA TU

Gazeti la Tanzania Daima lemieripoti kuwa Serikali imeanza uhakiki wa vyeti vya ndoa kwa watumishi wa umma. Hatua hiyo ambayo imewashtua watumishi wengi wa umma, imeelezwa kuwa ni mwendelezo wa harakati za Serikali ya Rais John Magufuli kuhakiki watumishi wa umma ili kuondokana na watumishi hewa.


Wakati Serikali ikianza na uhakiki wa vyeti vya ndoa, kazi ya uhakiki wa watumishi hewa na vyeti vyao vya elimu inaendelea sehemu mbalimbali nchini. 
Kwa muhibu wa Gazeti la Tanzania Daima habari ambazo limezipata zinasema kuwa serikali imeanzisha uhakiki huo nchi nzima kwa madai kuwa baadhi ya watumishi wa umma wamekuwa wakitoa taarifa za uongo kwamba wana ndoa ili kupata nauli na stahiki zingine za likizo wakati hawana ndoa.
Habari zaidi zinasema kuwa walimu wakuu wa shule zote za Wilaya ya Ilala wamepewa siku mbili kutekeleza agizo hilo kwa walimu wao. Mmoja wa walimu hao ambaye ameomba jina lake lihifadhiwe, alilithibitishia Tanzania  daima kuwa ametoa siku mbili kwa walimu wa shule yake wenye vyeti vya ndoa waviwasilishe kwake.
>>>’Kweli tumepewa agizo hilo leo manispaa ya Ilala na tumetakiwa kuwasilisha vyeti hivyo kesho na tayari baadhi ya walimu wangu wamefanya hivyo leo na kesho zoezi hilo linakamilika
Alipoulizwa sababu ya kuwepo kwa zoezi hilo, mwalimu huyo alisema hajui lakini anahisi lina lengo la kudhibiti taarifa za uongo za watumishi wakati wa kuomba likizo.
Wakati walimu wa shule za Ilala wakitakiwa kuwasilisha vyeti vyao vya ndoa, wilaya nyingine za Temeke, Kinondoni, Ubungo na Kigamboni hawana taarifa hizo.
Mmoja wa walimu kutoka Manispaa ya Ilala alisema kuwa uhakiki huo una lengo la kutaka kuchelewesha zaidi malipo na stahiki za walimu za likizo ambazo hazijalipwa kwa miaka mingi.

Friday, September 16, 2016

KIJANA ANYOFOLEWA ULIMI NA MKE WA JIRANI YAKE WAKATI WAKILA DENDA

Kijana mkazi wa Unyakhae nje kidogo ya mji wa Singida, Said Mnyambi (26) amelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Singida baada ya kunyofolewa kipande cha ulimi wake na mke wa jirani yake aliyekuwa anamlazimisha kufanya nae mapenzi.
Kwa mujibu ya maelezo ya kijana huyo, tukio hilo limetokea siku ya Idd El Haji Jumatatu wiki hii saa 3:30 usiiku.Alieleza kuwa siku ya tukio, mke wa jirani yao mmoja ambaye hakutaka kumtaja jina lake, alimwomba amsindikize nyumbani kwa kuwa amelewa .
Alidai walipofika njiani,mama huyo alimtaka wafanye naye mapenzi jambo ambalo kijana huyo alimkatalia lakini alimwomba angalau waagane kwa kunyonyana ulimi (denda) naye akamkubalia.
Nilimkubalia kumpa denda na hapo ndipo alipoanza kufungua mkanda wa suruali yangu, lakini nilipomkatalia kufungua mkanda wangu hapo ndipo alipong’ang’ania ulimi wangu hadi akanyofoa kipande na yeye akakimbilia kwake’;- Said Mnyambi
Alipoulizwa iwapo mama huyo ni mpenzi wake, kijana huyo alikataa kata kata na kujitetea kuwa alimuomba amsindikize kwa vile tu anamfahamu na ni jirani yake.
Mganga mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Singida, Dk Ramadhani Kabala alithibisha kunyofolewa kwa kipande cha ulimi wa kijana huyo na kueleza kuwa alifika hospitalini hapo kwa matibabu baada ya ulimi wake kupata maambukizi na kuingia usaha hadi kushindwa kuongea.
Source Habari Leo

Thursday, August 18, 2016

TPB YAWAMEGEA TIMU YA WAANDISHI WA HABARI ZA MICHEZO SHILINGI MILIONI MBILI

MAJU3
Afisa Habari na Mawasiliano wa benki ya Posta Tanzania (TPB), Chichi Banda akizungumza mara baada ya kukabidhi hundi ya sh Milioni 2 kwa Mwenyekiti wa Timu ya Waandishi wa Habari za Michezo nchini, Majuto Omary kwa ajili ya ziara ya mkoani Arusha kwa ajili ya kushiriki tamasha la waandishi wa habari wa mikoa ya Kanda ya Kaskazini
MAJU1
Afisa Habari na Mawasiliano wa benki ya Posta Tanzania (TPB), Chichi Banda akikabidhi mfano wa hundi kwa Mwenyekiti wa Timu ya Waandishi wa Habari za Michezo nchini, Majuto Omary kwa ajili ya ziara ya mkoani Arusha kwa ajili ya kushiriki tamasha la waandishi wa habari wa mikoa ya Kanda ya Kaskazini
Na Mwandishi wetu
Benki ya Posta Tanzania (TPB) imeendelea kuisadia timu ya   Waandishi wa habariza michezo  nchini (Taswa SC) baada ya kuikabidh  Sh milioni 2 kwa ajili ya kufanikisha safari yao ya kwenda mkoani Arusha kushiriki katika tamasha la Waandishi.
Akizungumza katika makabidhiano hayo, Afisa Mawasiliano wa Benki ya Posta Tanzania (TPB) Chichi Banda alisema kuwa msaada huo ni sehemu ya shughuli za Benki na kutambua mchango mkubwa wa Waandishi wa Habari Nchini.
Chichi alisema kuwa wamefariji kakutoa msaada huo kwaTaswa SC ambayo inakwendakuteteaubingwa wake katika tamashahiloambaloufanyika kila mwaka. Chichi alisema kuwa hii nimara ya tatu kwa TPB kuisaidiatimu hiyo.
Awali TPB ilikabidhi timu hiyo vifaa vya michezo napesa kwa ajili ya ziaraya mkoani Arusha na kufanikiwa kufanya vyema katika ziara hiyo kwa kuutwaa ubingwa ambao ina kwenda kuutetea mwaka huu.
“Waandishi wa habari wameonyesha mfano mkubwa kwa kucheza soka na netiboli, wameamua kuhamasisha michezo katika jamii, kwa vitendo, hii imetupa faraja kubwa sana kwetu, ”alisema Chichi.
Mwenyekiti waTaswa SC, MajutoOmaryaliishukuru TPB kwa kuendelea kuwakumbuka na kuahidi kutumia pesa hizo kwa ajili ya kufanikisha ziara yao katika maadhimisho ya tamasha la waandishii wa Habari jijini Arusha.
“Tunajivunia uwepo wa Benki ya Posta kwa kuthibitisha kuwa ni benki halisi ya Watanzania, nachukua fursa hii kuwaomba Watanzania kufungua akaunti zao katika benki hii na vile vilekuomba wadau wengine kufuata  mfano  kwa kuisaidiaTaswa SC ili iweze kufanikisha ziara zake,” alisema Majuto.
Majuto alisema kuwa bado timu yao inahitaji msaada zaidi ili kufanikisha ziara hiyo ambayo itawajumuisha wachezaji wa soka na netiboli. “Tunaishukuru Benki ya Posta, pia tunawaomba wadau wengine nao waunge mkono, muda bado upo,” alisema. (P.T)

Sunday, August 14, 2016

MGOSI ASTAAFU SOKA SASA KUWA MANAGER WA TIMU


 Mshambuliaji wa soka wa timu ya  Simba, Mussa Hassan Mgosi, akiwa na mwanawe, mara baada ya kucheza dakika tatu uwanjani kwenye pambano la soka la kirafiki baina ya timu yake na URA ya Uganda kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam, Agosti 14, 2016. , na kustaafu soka  Mgosi aliyechezea simba kwa misimu 10 amestaafu soka na sasa atakua meneja wa timu hiyo. Miongoni mwa watu waliohudhuria sherehe hiyo ya kustaafu kwake, ni pamoja na Familia yake, mkewe Jasmin na watoto wake watatu. Katika pambano hilo la kirafiki baina ya Simba na URA, matokeo yamekuwa sare ya kufungana magoli  1-1. (PICHA NA K-VIS B;LOG/KHALFAN SAID)
gosi
 Mgosi akikokota mpira mbele ya mchezaji wa URL kwenye pambano la soka la kirafiki kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam, Agosti 14, 2016

 Familia ya Mgosi ikiongozwa na mkewe Jasmina, (katikati) na watoto wake, Amina (kushoto) na Hassan wakipiga makofi baada ya Mgosi kustaafu soka kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam

 Mchezaji wa Kimataifa wa Simba, Laudit Mavugo, akiipasua ngome ya URL

 Ibrahim Ajib, akikokota mpira

Friday, June 26, 2015

HISA ZA CRDB KUANZA KUUZWA JUNI 26

 Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa akifungua mkutano wa wanahisa wa benki hiyo katika Hoteli ya Sea Cliff jijini Dar es Salaam.
 Katibu wa Benki ya CRDB, John Rugambwa akizungumza wakati wa mkutano wa wanahisa uliofanyika katika hoteli ya Sea Cliff jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti waBodi yaWakurugenzi ya Benki ya CRDB, Martin Mmari akizungumza katika mkutano huo.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei, akizungumza na baadhi ya wanahisa wa benki hiyo kuhusu kuanza rasmi kwa mchakato wa uuzaji wa hisa stahili za benki hiyo unaoanza Juni 26 hadi Julai 16. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam.
  Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei, akizungumza na baadhi ya wanahisa wa benki hiyo kuhusu kuanza rasmi kwa mchakato wa uuzaji wa hisa stahili za benki hiyo unaoanza Juni 26 hadi Julai 16. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam. 
 Baadhi ya maofisa wa benki hiyo pamoja na wanahisa wakimsikiliza Dk. Charles Kimei.
 Baadhi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB. 
 Wakurugenzi wa Benki ya CRDB na wanahisa wakiwa katika mkutano huo.
 Baadhi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB na mameneja wa matawi wakiwa katika mkutano huo.
Meza Kuu.

 Dar es Salaam, Tanzania
BENKI ya CRDB, imetangaza kuanza rasmi kwa mchakato wa uuzaji wa Hista Stahili kwa wanahisa wake, unaofunguliwa Juni 26 na kuhitimishwa Julai 16, ili kuongeza mtaji wake wa uendeshaji.
Hisa Stahili ni zile za ongezeko zinazotolewa au kuuzwa kwa wanahisa wa benki hiyo kwa mfumo wa hisa moja mpya kwa kila hisa tano anazomiliki.
Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa mauzo hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB, Dk. Charles Kimei, alisema kuwa baada ya maazimio ya wanahisa wake wote katika Mkutano Mkuu uliopita.
“Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, imeidhinisha kuingiza sokoni hisa mpya 435,306,432 kwa ajili ya wanahisa wake ambapo kila hisa moja itauzwa kwa shilingi 350, hivyo kusanyo tarajiwa la mtaji mpya litakuwa ni sh. 152,357,251,200,” alisema Dk. Kimei.
Alibainisha kuwa fedha hizo zitakazopatikana baada ya mauzo ya hisa zitatumika kwa mambo kadhaa, ikiwamo uboreshaji wa njia za kutolea huduma kwa wateja wa benki hiyo.
“Mwanahisa atakayekuwa na sifa za kupokea kupokea hisa hizi ni yule tu atakayekuwa kwenye kumbukumbu za vitabu vya benki mpaka kufikia Alhamisi Juni 18 mwaka huu ambayo ilikuwa siku ya mwisho ukusanyaji kumbukumbu hizo,” alifafanua Dk. Kimei.
Aliongeza kuwa CRDB inahitaji kuongeza mtaji wake ili kufikia malengo yake ya kibiashara, ikiwamo upanuzi wa mtandao na ununuzi mitambo ya uendeshaji.

“CRDB imeona hii ndio njia sahihi na bora zaidi, kwani licha ya kuongeza mtaji, pia inatoa fursa kwa wanahisa wetu kuongeza hisa zao sambamba na umiliki wao wa benki hii,” alibainisha Dk. Kimei.
 Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa akifungua mkutano wa wanahisa wa benki hiyo katika Hoteli ya Sea Cliff jijini Dar es Salaam.
 Katibu wa Benki ya CRDB, John Rugambwa akizungumza wakati wa mkutano wa wanahisa uliofanyika katika hoteli ya Sea Cliff jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti waBodi yaWakurugenzi ya Benki ya CRDB, Martin Mmari akizungumza katika mkutano huo.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei, akizungumza na baadhi ya wanahisa wa benki hiyo kuhusu kuanza rasmi kwa mchakato wa uuzaji wa hisa stahili za benki hiyo unaoanza Juni 26 hadi Julai 16. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam.
  Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei, akizungumza na baadhi ya wanahisa wa benki hiyo kuhusu kuanza rasmi kwa mchakato wa uuzaji wa hisa stahili za benki hiyo unaoanza Juni 26 hadi Julai 16. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam. 
 Baadhi ya maofisa wa benki hiyo pamoja na wanahisa wakimsikiliza Dk. Charles Kimei.
 Baadhi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB. 
 Wakurugenzi wa Benki ya CRDB na wanahisa wakiwa katika mkutano huo.
 Baadhi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB na mameneja wa matawi wakiwa katika mkutano huo.
Meza Kuu.

 Dar es Salaam, Tanzania
BENKI ya CRDB, imetangaza kuanza rasmi kwa mchakato wa uuzaji wa Hista Stahili kwa wanahisa wake, unaofunguliwa Juni 26 na kuhitimishwa Julai 16, ili kuongeza mtaji wake wa uendeshaji.
Hisa Stahili ni zile za ongezeko zinazotolewa au kuuzwa kwa wanahisa wa benki hiyo kwa mfumo wa hisa moja mpya kwa kila hisa tano anazomiliki.
Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa mauzo hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB, Dk. Charles Kimei, alisema kuwa baada ya maazimio ya wanahisa wake wote katika Mkutano Mkuu uliopita.
“Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, imeidhinisha kuingiza sokoni hisa mpya 435,306,432 kwa ajili ya wanahisa wake ambapo kila hisa moja itauzwa kwa shilingi 350, hivyo kusanyo tarajiwa la mtaji mpya litakuwa ni sh. 152,357,251,200,” alisema Dk. Kimei.
Alibainisha kuwa fedha hizo zitakazopatikana baada ya mauzo ya hisa zitatumika kwa mambo kadhaa, ikiwamo uboreshaji wa njia za kutolea huduma kwa wateja wa benki hiyo.
“Mwanahisa atakayekuwa na sifa za kupokea kupokea hisa hizi ni yule tu atakayekuwa kwenye kumbukumbu za vitabu vya benki mpaka kufikia Alhamisi Juni 18 mwaka huu ambayo ilikuwa siku ya mwisho ukusanyaji kumbukumbu hizo,” alifafanua Dk. Kimei.
Aliongeza kuwa CRDB inahitaji kuongeza mtaji wake ili kufikia malengo yake ya kibiashara, ikiwamo upanuzi wa mtandao na ununuzi mitambo ya uendeshaji.

“CRDB imeona hii ndio njia sahihi na bora zaidi, kwani licha ya kuongeza mtaji, pia inatoa fursa kwa wanahisa wetu kuongeza hisa zao sambamba na umiliki wao wa benki hii,” alibainisha Dk. Kimei.

Thursday, June 25, 2015

ZITTO AKAGUA SOKO KUU WILAYANI MASASI LILOTEKETEA KWA MOTO

1
Kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, akimsikiliza Mwenyekiti wa Soko Kuu wilayani Masasi Mkoani Mtwara, Abdallah Mandoma, lililoteketea kwa moto usiku wa kuamkia jana, mjini humo ambapo  chanzo cha moto huo kimeelezwa ni hitilafu ya umeme.
2
Kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, akisaidia kuzima moto ambao uliteketeza Soko Kuu la Masasi Mkoani Mtwara, usiku wa kuamkia jana wafanyabiashara zaidi ya 1000 wamepata hassara.
…………..
AJALI
mail.google.com
Kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, akisalimiana na askari aliposhuka kuwapa pole abiria waliopata ajali eneo la Kata ya Mtua Kijiji cha Kilimahewa A, Mkoani Lindi jana, ambapo watu wawili walipoteza maisha. Chanzo cha ajali hiyo ni dereva wa basi akijaribu kumkwepa muendesha baskeli. (DK)
45
Kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, akizungumza na wananchi wa eneo ilipotokea ajli hiyo.

Monday, June 22, 2015

HII NDIYO KAULI YA WASIRA AMBAYE ANATARAJIA KUGOMBEA URAIS KATIKA MAJIBU YAKE KUHUSI WINGI WA WAGOMBEA URAIS KUTOKA CCM

36593
Watu ambao tayari wamejitokeza kutangaza kwamba Wanagombea nafasi ya kuwa wawakilishi wa CCM kwenye nafasi ya Urais idadi yao ni zaidi ya 35 mpaka sasa hivi... Waziri Steven Wasira amewasha kipaza sauti ndani ya Kikao cha Bunge Dodoma na kuongea hizi sentensi zake chache tu kwa wanaokosoa idadi hiyo ya Wagombea.
“Chama cha Mapinduzi ni Chama kikubwa wengine wako huko wananung’unika ooh kina Wagombea wengi mlitaka wawe wachache ili wawe wangapi? Ni wengi kwa sababu Chama chenyewe ni kikubwa, sio Chama kidogo ambacho Viongozi wake wakiingia kwenye Helicopter chini kunabaki hakuna Kiongozi” Steven Wasira.
“Tunapashapasha moto alafu mwisho wa yote tunapata Mgombea mmoja na tutasonga mbele, mwendelee kujiandaa kuwa Wapinzani” Waziri Steven Wasira.
Sauti ya Waziri Steven Wasira iko hapa.

WAMASAI WAONYESHA DALILI YA KUACHA UKEKETAJI

Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues (kushoto) akimpongeza Kiongozi Mkuu wa Jamii ya Kimasai Afrika Mashariki, Mokombo Olaiboni Simeli kwenye semina ya viongozi mbalimbali wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi wa shule za msingi na sekondari Wilayani Ngorongoro, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilaya ya Ngorongoro.
Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues (kushoto) akimpongeza Kiongozi Mkuu wa Jamii ya Kimasai Afrika Mashariki, Mokombo Olaiboni Simeli kwenye semina ya viongozi mbalimbali wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi wa shule za msingi na sekondari Wilayani Ngorongoro, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilaya ya Ngorongoro.
Susana Koillah, Mama Shughuli na mtafsiri wa lugha ya Kimasai katika semina hiyo akimsikiliza kwa makini Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues (kulia) kabla ya kutafsiri mada yake kwa wanasemina.
Susana Koillah, Mama Shughuli na mtafsiri wa lugha ya Kimasai katika semina hiyo akimsikiliza kwa makini Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues (kulia) kabla ya kutafsiri mada yake kwa wanasemina.
Sehemu ya washiriki wa semina ya viongozi wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi wa shule za msingi na sekondari, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilayani Ngorongoro wakiwa kwenye semina hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro juzi.
Sehemu ya washiriki wa semina ya viongozi wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi wa shule za msingi na sekondari, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilayani Ngorongoro wakiwa kwenye semina hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro juzi.
Ofisa HIV na Elimu ya Afya Taifa wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Mathias Herman (kushoto) akitoa maelekezo kwa wana semina ya viongozi wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi shule za sekondari, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilayani Ngorongoro wakiwa kwenye semina hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro juzi.
Afisa mradi wa Elimu ya Afya na VVU/UKIMWI Taifa wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Mathias Herman (kushoto) akitoa maelekezo kwa wana semina ya viongozi wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi shule za sekondari, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilayani Ngorongoro wakiwa kwenye semina hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro juzi.
Sehemu ya washiriki wa semina ya viongozi wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi wa shule za msingi na sekondari, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilayani Ngorongoro wakiwa kwenye semina hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro juzi.
Sehemu ya washiriki wa semina ya viongozi wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi wa shule za msingi na sekondari, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilayani Ngorongoro wakiwa kwenye semina hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro juzi.
VIONGOZI wakuu wa jamii ya Kimasai wa Afrika Mashariki wameridhia kuachana na mila potofu zimezopitwa na wakati ikiwemo vitendo vya ukeketaji kwa wasichana wa jamii ya kimasai ambavyo vimekuwa vikiwaathiri wasichana hao kwa kiasi kikubwa.
Kauli ya kusitisha vitendo hivyo ilitolewa juzi Wilayani Ngorongoro na Kiongozi Mkuu wa Jamii ya Kimasai Afrika Mashariki, Mokombo Olaiboni Simeli pamoja na msaidizi wake kutoka Tanzania, Sangau Naimado Olaiboni walipokuwa katika semina ya elimu ya afya ya uzazi, kupinga vitendo vya ukeketaji pamoja na mimba za utotoni.
Kiongozi Mkuu wa Jamii ya Wamasai Afrika Mashariki, Olaiboni Simeli alimueleza Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) na Mwakilishi wa Shirika hilo Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues kuwa jamii hiyo ya wamasai imeridhia kuacha mila zilizopitwa na wakati na itaendelea kushiriki kuelimisha jamii yao zaidi juu ya madhara ya mila hizo potofu ikiwemo ukeketaji na ndoa za utotoni.
“…Tunaishukuru UNESCO kwa kuendelea kutoa elimu hii kwetu juu ya mila potofu nasisi tunaungana nanyi kuendelea kutoa elimu kwa jamii yetu kupinga ukeketaji na ndoa za utoto tumeelezwa athari nyingi zinazowapata wasichana wanaokeketwa…kwanini tuendelee na mila zinazoleta madhara kwa watu wetu? Tushirikiane kupiga vita hivi,” alisema Olaiboni Simeli akizungumza mbele ya Bi. Rodrigues.
Kwa upande wake Kiongozi Mkuu wa Jamii ya Wamasai Tanzania, Naimado Olaiboni alisema hakuna haja ya jamii ya kimasai kuendelea na mila zilizopitwa na wakati ilhali mila hizo zikiendelea kuwaathiri wamasai na kuwabakiza nyuma kimaendeleo katika nyanja mbalimbali. “…Tutaendelea kushirikiana nanyi kupinga ndoa za utotoni kwa kuwa tumeelezwa madhara yake na wataalamu leo,” alisema Naimado Olaiboni.
Naye Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la UNESCO Tanzania, Bi. Rodrigues alisema anapenda kuona Jamii ya Kimasai inaendeleza mila na tamaduni zao lakini zile nzuri ambazo hazina chembe ya kiunyanyasaji kwa makundi yote. Alisema ukeketaji kwa wasichanga unamadhara makubwa kwa jamii hiyo hivyo haina budi mila hizo kupuuzwa ili kumlinda mtoto wa kike na madhara yanayomkumba anapofanyiwa vitendo hivyo.
“…Napenda kuona Wamasai wanaendeleza mila na tamaduni zao lakini ziwe nzuri na zisizo na chembe ya ukatili wala unyanyasaji, tuangalie ni namna gani tunaziendeleza na kubaki katika uhalisia wetu…nawahakikishia tutashirikiana kuhakikisha hili linafanikiwa kwenu,” alisema Bi. Rodrigues akizungumza katika semina hiyo.
Aidha aliwashauri jamii ya Kimasai kupunguza kuwa na idadi kubwa ya watoto na wake ilhali mume akishindwa kuihudumia familia hiyo jambo ambalo limeendelea kuchochea umaskini wa familia hizo vijijini kwani watoto wamekosa mahitaji ya msingi katika familia na kujikuta wakiishi kwa taabu.
Aliwataka Wamasai pia kupinga ndoa za utotoni kwani mabinti wadogo wanapoolewa wanakosa fursa ya elimu pamoja na kuunda familia bora kutokana na uduni wao katika masuala ya afya ya uzazi kiujumla na madhara yanayowaandama katika maisha yao. “…Ndoa za utotoni nazo ni tatizo katika jamii yetu, tuzipige vita maana mtoto mdogo anapoolewa haweza kuunda familia bora na wala uzazi wake hauwezi kuwa bora…,” aliongeza Bi. Rodrigues.
Zaidi ya wanasemina 210 kutoka Kata za Ololosokwani, Arash, Soit Sambu, Oloipili, Aoliani Magaidulu wakiwemo viongozi mbalimbali wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi wa shule za msingi na sekondari na wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii Wilayani Ngorongoro wamenufaika na semina hiyo ya jitihada za kuelimisha jamii juu ya mila na desturi zilizopitwa na wakati.