Monday, October 6, 2014

HII NDIO ILE SHEREHE YA MIAKA 24 YA JAMUHURI YA MUUNGANO WA UJERUMANI: ANDY CHANDE WA FREEMASON ALIKUWEPO

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Ujerumani nchini Tanzania, Egon Kochanke (katikati) na mkewe Wendy Marshall Kochanke wakimkaribisha mfanyabiashara mashuhuli Sir Andy Chande katika tafrija ya kusherehekea Miaka 24 ya Jamhuri ya Muungano wa Ujerumani, iliyofanyika nyumbani kwa Balozi huyo, Kenyatta Drive Oysterbay jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki. PICHA ZOTE/JOHN BADI WA DAILY MITIKASI BLOG

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Ujerumani nchini Tanzania, Egon Kochanke (kulia) na akikaribisha wageni katika tafrija ya kusherehekea Miaka 24 ya Jamhuri ya Muungano wa Ujerumani, iliyofanyika nyumbani kwa Balozi huyo, Kenyatta Drive Oysterbay jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki. 

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Ujerumani nchini Tanzania, Egon Kochanke (kulia), akimkaribisha Mwenyekiti wa Mwalimu Nyerere Foundation, Joseph Butiku wakati wa tafrija hiyo.(P.T)

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Ujerumani nchini Tanzania, Egon Kochanke (katikati) na mkewe Wendy Marshall Kochanke wakimkaribisha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe ambaye alikuwa mgeni rasmi katika tafrija hiyo. 

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Ujerumani nchini Tanzania, Egon Kochanke akisoma hotuba yake.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe akisoma hotuba yake. 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Ujerumani nchini Tanzania, Egon Kochanke wakigonganisha glasi kama ishara ya kusherehekea tafrija hiyo. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Ujerumani nchini Tanzania, Egon Kochanke na mke wa Balozi wakikata keki maalum  kama ishara ya kusherehekea tafrija hiyo. 

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Ujerumani nchini Tanzania, Egon Kochanke akipata ukodak na baadhi ya wageni waalikwa.
 
Mambo ya Ukodak, John Merkion na Dada mkubwa bila yeye no visa wakishow love.

Muziki mkubwa uliporomoshwa na Bendi ya Wakwetu Vibes kutoka pande za Mikocheni.



Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Ujerumani nchini Tanzania, Egon Kochanke akiwa katika picha ya pamoja na kikosi kazi cha ubalozi huo.  

No comments:

Post a Comment