Monday, April 14, 2014

HII NI KUFURU: KILA MGENI MUALIKWA ALIYEHUDHURIA HARUSI YA MTOTO WA WA RASI , AMEPEWA "IPHONE 5 NA TABLET ZA DHAHABU" TAZAMA PICHA HAPA

     

Kibongo bongo tumezoea mtu anapotaka kufunga ndoa lazima ipitishwe michango ya kutosha ili kuweza kufanikisha sherehe, na pia mchango wako ndio huwa kiingilio chako yaani bila kuchanga hupati mwaliko. 

Hizi ni zawadi za iPhone 5 walizopewa wageni waalikwa

Mambo yamekuwa kinyume katika harusi ya mtoto wa kike wa Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria aitwaye Faith, ambaye katika harusi yake iliyofanyika jana (April 12) wageni walioalikwa wamefanyiwa surprise kwa kupewa zawadi ya simu za iPhone 5 ‘gold plated customized’, zilizoandikwa majina ya maharusi hao Faith na Godswill.

Juu ya mabox yaliyokuwa na zawadi ya simu hizo pameandikwa ‘Leeberry and her Prince wish you all the best for making our day beautifull. Thanx for coming and God Bless you’
Cha kusikitisha ni kwamba aina ya wageni wanaoweza kupata mwaliko wa harusi kama hii ya mtoto wa mkubwa ni watu wa class flani ya watu wanaojiweza, hivyo unaweza kukuta ni mtu ambaye tayari anayemiliki hata iPhones mbili au tatu, so inakuwa sio big deal kivile! (Nawaza tu kwa sauti).
>>Naija Gists

No comments:

Post a Comment