Mkutano wa Baraza la wafanyakazi wa Wizara ya Nishati na
Madini , uliokuwa ukijadili Bajeti ya Mwaka 2013/2014, umefungwa jana na Naibu waziri wa Wizara hiyo Mhe Steven Maselle Katika
Hoteli ya Bluer Pearl jijini Dar es Salaam.
Wakati akifunga, Mkutano huo, Mhe, Maselle amewapongeza wajumbe wa
Baraza la mkutano huo kwa kuongeza mapato ya
Bajeti kwa mwaka huu ambapo
yamefikia wastani wa 75% tofauti na ilivyokuwa mwaka jana
ambapo mapato yalikuwa chini ya asilimia 75%.
Amesema kuwa eneo la Madini ni moja ya Sekta iliyofanikiwa kukuza Bajeti ya mwaka huu kwani, wameongeza Mapato zaidi .
“Niwapongeze sana kwa kuwa Bajeti ya Wizara yetu sasa
imekuwa tofauti na Wizara Zingine jambo ambalo linatupa faraja sisi viongozi
hivyo endeleeni na Moyo huohuo wa kuweza kuhakikisha uchumi wa Tanzania Unakua
kwa kasi.
Miongoni Mwa Agenda zilizo Zungumziwa katika kikao hicho ni
pamoja na namna ya Kuboresha Utendaji wa Wizara, Namna ya kuhakikisha Uchumi wa
Taifa unakua kwa kasi, na kuhakikisha kuwa nishati ya umeme inapatikana ya
uhakika ambapo wamekubaliana kuwekeza
katika miundombinu ya Usafirishaji wa
Umeme ili kuhakikisha kuwa Watanzania wanafurahia Nishati ya umeme hapo Baadae.
No comments:
Post a Comment