MKUU
wa Wilaya ya Igunga, Tabora Elibariki Kingu, amemuondoa Mkurugenzi
Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Majitaka na kumrejesha kwa Mwajili
wake kutokana na kushindwa kwake kusimamia Mradi wa maji katika Bwawa la
Bulenya.
Akizungumza na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam
jana, Kingu alisema alikwisha mwandikia barua Mkurugenzi huyo, Lema
Jeremia, ambapo alisisitiza kuwa barua hiyo si ya kumfukuza kazi bali ni
ya kumuondoa wilayani kwake.
“Kazi hii alipewa Mkandarasi
anayeitwa Wessons Tanzania Limited, mradi huu ulikuwa ni lot No. IG14 na
mkataba namba IDC/CF/T/04/05/29, ambapo mkataba ulisainiwa Julai 29,
2008 huku muda wa utekelezaji ukiwa ni miezi sita lakini hadi leo ni
miaka mitano mradi huo haujakamilika”alisema Kingu.
Alisema mkurugenzi huyo
alifumbia macho matatizo ya maji katika wilaya hiyo, kusababisha
Serikali ishindwe kutimiza ahadi zake kikamilifu kwa wananchi na kwa
makusudi alisaini cheki za malipo wakati akitambua wazi hakuna mradi
uliokamilika.
Kingu alisema mradi huo
uliotengewa sh bilioni 1.94 kwa ajili ya kuengeneza miundombinu ya vituo
vya kusambaza maji katika wilaya hiyo.
Alisema mradi huo ulitarajiwa
kukamilika Januari 2009, cha kushangaza hadi mwaka huu wa 2013,
mkandarasi amelipwa zaidi ya asilimia 95 ya fedha ambazo ni sh milioni
9.7 huku akiwa hajakabidhi kazi.
“Baada ya uamuzi huo,
nimeviagiza vyombo vya dola hususan Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na
Rushwa (TAKUKURU), kukamilisha haraka uchunguzi na kumfungulia mashitaka
mara moja”alisema Kingu
Kingu alibainisha kuwa vituo
tisa kati ya 13 ambavyo vilipaswa kutoa maji vimetelekezwa na havitoi
maji ambapo alivitaja kuwa ni NMB, Kwa Mzee Costa,Masanga, CCM, Kilabu
cha China, Kamando, Kokoto, Mwayunge na Mnadani.
“Hili nitalifanyia kazi na wala
sitamuogopa mwananasiasa yeyote hata kama ni kupoteza kazi niko tayari,
lakini siko tayari kufukuzwa kazi kwa ajili ya uzembe wa mtu mwingine
anayeshindwa kutimiza majukumu yake, kwa ajili ya manufaa ya
wananchi”alisema Kingu.
Alipotafutwa Jeremia, ili kutoa
ufafanuzi kuhusu kauli ya Mkuu wa Wailaya huyo, alikiri kupokea barua
hiyo hata hivyo, alisema kuchelewa kwa mradi huo kunatokana na mwaajili
wake kuchelewa kulipa fedha za mradi huo kwa wakati.
Vilevile
alisema hakuna fedha zilizolipwa nje ya kazi, amabapo pia alidai kuwa
mradi huo hadi sasa umekamilika kwa zaidi ya asilimia 90.
No comments:
Post a Comment