Friday, March 1, 2013

Milipuko miwili yaua 3 huko Mogadishu

Watu wasiopungua watatu waliuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa siku ya Ijumaa (tarehe 1 Machi) katika mashambulio mawili kwenye mgahawa ulio katika fukwe za mbele maarufu huko Mogadishu, AFP iliripoti.

Milipuko hiyo iliripotiwa kusababishwa na washambuliaji wa kujitoa muhanga waliovaa fulana zilizosheheni milipuko, ikifuatiwa na bomu la gari.
"Mwanaume huyo alijilipua wakati walinzi wa lango la mgahawa walipokuwa wakijaribu kumzuia… takriban watu watatu pamoja na mlipuaji walikufa," alisema Hersi Adan, kiongozi wa usalama ambaye alikuwepo karibu na tukio la shambulizi.
"Dakika chache baadaye gari liliegeshwa nje ya jengo hilo lililipuka na kuua mwingine na kujeruhi watu saba," alisema.
Mlipuko huo ulitokea karibu na ufukwe maarufu wa Lido huko Mogadishu, ambao kwa kawaida hujaa watu siku za wikendi pamoja na familia zikifurahia ufukwe, kucheza mpira wa miguu au kuogelea katika Mawimbi ya Bahari ya Hindi.
Hakuna kikundi kilichodai kwa haraka kuhusika na mlipuko huo, lakini al-Shabaab imezindua mfululizo wa mashambulizi ya mtindo wa vita vya msituni huko Mogadishu katika miezi ya hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment