Saturday, March 16, 2013

MATOKEO YA UCHAGUZI WA WENYEVITI NA MAKAMU WENYEVITI WA KAMATI ZA BUNGE


1
Katibu wa Bunge Ndg. John Joel akitangaza Matokeo ya wenyeviti na Makamu wa Wenyeviti mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi wa viongozi hao katika kamati zote za Bunge leo. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa kamati za Bunge Ndg. Theonist Luhirabake na kulia ni Afisa Habari wa Bunge Ndg. Owen Mwandumbya13Wajumbe wa Kamati ya PAC wakiteta na Mhe. John Cheyo anaye tetea kiti chake cha uenyekiti wa kamati 15Mhe. David Kafulila akimpongeza Mhe. James Lembeli mara baada ya kupita bila kupingwa kwa nafasi ya uenyekiti wa kamati ya Ardhi  Maliasili na Mazingira 
5. Msimamizi wa Uchaguzi katika kamati ya Mambo ya Nje na Uhusiano wa kimataifa Bi. Justina Shauri akiwapa maelezo ya awali wajumbe wa kamati hiyo kabla ya kuchagua viongozi wao.  Msimamizi wa Uchaguzi katika kamati ya Ulinzi na Usalama Ndg. Peter Magati akiwapa maelezo ya awali wajumbe wa kamati hiyo kabla ya kuchagua viongozi wao.
8Katibu wa Kamati ya PAC Bi. Lina Kitosi ambaye pia ndiye msimamizi wa uchaguzi akiwaonesha wajumbe wa kamati hiyo karatasi maalum ya kupigia kula kabla ya uchaguzi kufanyika
9Mgombea nafasi ya Uwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) Mhe. Zitto Kabwe akinadi sera zake mbele ya wajumbe wa kamati hiyo kabla ya kufanyika kwa uchaguzi leo
12Mgombea wa Nafasi ya Uenyekiti katika kamati ya LAAC Mchungaji Israel Natse nae akinadi sera zake

No comments:

Post a Comment