Baadhi
ya viongozi wa dini waliohudhuria sherehe za miaka 25 ya hospitali ya
Hubert Kairuki Mikocheni, Dar es salaam, leo Machi 16, 2013. PICHA NA IKULU
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi
tuzo kwa kutambua mchango wake mkubwa katika sekta ya afya nchini wakati
wa sherehe za miaka 25 ya hospitali hiyo leo Machi 16, 2013
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wakati wa sherehe za miaka 25 ya
hospitali ya Kumbukumbu ya Hubert Kairuki Mikocheni, Dar es salaam, leo
Machi 16, 2013
Msanii
Mrisho Mpoto akiburudisha wakati wa sherehe za miaka 25 ya hospitali ya
Hubert Kairuki Mikocheni, Dar es salaam, leo Machi 16, 2013
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wengine wakikata utepe kuzindua rasmi
hosteli ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Hubert Kairuki
wakati wa sherehe za miaka 25 ya hospitali ya Hubert Kairuki Mikocheni,
Dar es salaam, leo Machi 16, 2013
Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi, Waziri Mkuu Mstaafu, Dkt Salim Ahmed Salim
wakiangalia watoto wachanga waliotunzwa katika chumba maalum muda mfupi
baada ya kuzaliwa wakati Rais Kikwete alipotembelea sehemu mbalimbali za
hospitali ya Kumbukumbu ya Hubert Kairuki akiwa mgeni rasmi katika
sherehe za miaka 25 ya kuanzishwa kwake leo Machi 16, 2013.
Mkurugenzi
Mkuu wa hospitali ya Kumbukumbu ya Hubert Kairuki, Mama Koku Kairuki
akimkabidhi tuzo Rais Jakaya Mrisho Kikwete kwa kutambua mchango wake
mkubwa katika kuendeleza sekta ya afya nchini wakati wa sherehe za miaka
25 ya hospitali hiyo leo Machi 16, 2013
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi, Waziri Mkuu
Mstaafu Dkt Salim Ahmed Salim, na viongozi wa hospitali ya Hubert
Kairuki wakiwa katika picha ya pamoja na vijana waliozaliwa
katika hospitali hiyo miaka 25 iliyopita leo Machi 16, 2013.
Seehemu ya wageni waalikwa na wanafunzi na wafanyakazi wa hospitali ya
Kumbukumbu ya Hubert Kairuki wakati wa sherehe za miaka 25 ya hospitali
ya Hubert Kairuki Mikocheni, Dar es salaam, leo Machi 16, 2013
No comments:
Post a Comment