Monday, March 4, 2013

MAHAKAMA YA SOMALYA YAMSWEKA MWANDISHI WA HABARI JELA...YAMWACHIA MWANAMKE ALIYEDAIWA KUBAKWA

Mahakama ya rufaa ya Somalia siku ya Jumapili (tarehe 3 Machi) ilfuta mashtaka dhidi ya mwanamke aliyehukumiwa kwenda jela mwaka mmoja baada ya kumwambia mwandishi wa habari kuwa alibakwa na vikosi vya usalama, lakini mwandishi wa habari ataendelea kubakia jela, AFP iliripoti.

"Mahakama hiyo iliamuru kuachiwa huru mwanamke huyo, huku mwandishi wa habari atabakia jela kwa miezi sita kwa kukosea taasisi za serikali," Jaji Hassan Mohamed Ali alisema. "Mahakama imejua kuwa mwandishi wa habari alimdanganya mshtakiwa anayedaiwa kubakwa ili kufanya mahojiano."
Mwezi uliopita, mwanamke, Lul Ali Osman, na mwandishi wa habari Abdiasis Abdinuur Ibrahim, mwenye umri wa miaka 25, walipatikana na hatia ya kukosea taasisi za serikali. Ibrahim pia alipatikana na kosa la "kufanya mahojiano ya uongo, na kuingia kwenye nyumba ya mwanamke huyo ambaye mumewe hakuwepo".
Osman, ambaye mwanzoni alitakiwa kukaa kwa miezi sita bila kumnyonyesha mwanaye mdogo kabla ya kuanza kutumikia kifungo chake cha jela, aliachiwa huru kutoka katika mahakama ya Mogadishu baada ya uamuzi huo kutolewa.
Lakini Ibrahim alifungwa pingu na kuingizwa kwenye lori lililomrudisha gereza kuu, kulikochochea majibizano ya hasira kutoka kwenye vikundi vya haki na wenzake.
Daniel Bekele, Mkurugenzi wa Afrika wa shirika la haki za binadamu la Human Rights Watch, alikosoa kuendelea kumtia ndani Ibrahim, ambaye amekuwa jela kutoka tarehe 10 Januari.
"Mahakama ya rufaa ilipoteza nafasi ya kufanyia haki kosa la kutisha, kwa mwandishi wa habari pamoja na kwa uhuru wa vyombo vya habari nchini Somalia," Bekele alisema katika taarifa. "Serikali imetoa wito kwa mahakama kuweka uelekeo wake katika kesi hii, lakini kila hatua haki imekiukwa"

No comments:

Post a Comment