Friday, January 11, 2013

HABARI NJEMA KWA WATU WA KILWA, KAMPUNI NNE ZA KIMATAIFA ZAWEKEZA KILWA.


Baadhi ya madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa ambao watatakiwa kuisimamia halmashauri hiyo ili kuhakikisha inakusanya mapato yote inayostahili kwenye vyanzo vyake na kuahakikisha mapato hayo yanatumika vizuri kwenye mgawanyo wa miradi ya maendeleo.


KASI ya maendeleo Wilayani Kilwa inatarajiwa kuongezeka kuanzia sasa baada ya Makampuni manne ya Kimataifa kuwekeza vitega uchumi Wilayani humo.

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Adoh Mapunda alisema halmashauri yake kwa sasa imezipokea kampuni nne za wawekezaji wapya wa kimataifa ambao wataongeza ajira kwa wakazi wa Kilwa na Tanzania kwa ujumla.

Mapunda aliyataja makampuni hayo na kiwango cha ajira kitakachotokana na makampuni hayo pamoja na hali ya kiuchumi itakavyokua kwa kasi.

Statoil Tanzania Ltd kutoka nchini Norway ambayo imegundua gesi na inatarajia kujenga mtambo mkubwa wa kuchakata gesi (Liquidified natural gas) kwenye kata ya Lihmalyao kwa gharama ya Tsh18Billioni na kutoa ajira zaidi ya 16,000.
 Kampuni nyingine ni Kilwa Energy Tanzania Ltd, itakayofua umeme na kuingiza kwenye gridi ya taifa kuanzia kwenye eneo la Somanga hadi Kinyerezi jijini Dar es Salaam. Kampuni hiyo inatarajiwa kuzalisha ajira za zaidi ya 800.

Kampuni nyingine ni ile ambayo imeshaanza uzalishaji kwenye eneo hilo la Kilwa ni ya Lee Cement Factory ambayo inatengeneza Saruji mjini Kilwa na kusababisha bei ya saruji Wilayani humo kushuka kutoka Tsh 18,000 hadi 13,000 ambapo kiwanda hicho kinauwezo wakutengeneza tani 8334 kwa mwezi.

Kampuni nyingine aliitaja kuwa ni Kaidi kutoka nchini China ambayo inawekeza kwenye kilimo na imepewa eneo la Ekari 13,000 kwenye vijiji vya Mitole na Ngea, ambako kutalimwa mazao mchanganyiko yakiwamo Mpunga, Mahindi, Mihogo, Miwa Mtama na matunda. Mbali na kilimo kampuni hiyo pia itazalisha umeme utakaotokana na takataka.

Adoh alisema halmashauri imeshapokea Tsh200Millioni ikiwa ni sehemu ya asilimia0.3 kutoka kwa kampuni ya kampuni ya gesi, ushuru wa  Tsh200,000 unaotokana na madini ya jasi yanayotengenezwa saruji.
Vyanzo hivyo vya pesa vitasaidia sana kuinua maendeleo Wilayani humo.

No comments:

Post a Comment