Kamishna mkuu wa sensa ya watu na makazi Bi Hajjat Mrisho akisisitiza jambo mbele ya waandishi wa habari leo katika makao makuu ya Ofisi za Takwimu jijini Dar es Salaam. |
Katika zoezi la Sensa lililoanza tarehe 26 Agosti 2012
ambalo lilikuwa limalizike leo limegonga mwamba baada ya kubainika kuwa kuna
watu chini ya asilimia tano ambao hawajahesabiwa hivyo Ofisi ya Takwimu kupitia
Kamishna wa Sensa ya watu na makazi amewatangazia
watanzania kuwa zoezi linaendelea,
kuandikisha watu wote wale ambao hawajaandikishwa hadi tarehe 8 septemba 2012 ili kila mwananchi apate
nafasi kwa tathmini iliyofanywa na ofisi ya Sensa.
Kamishna wa Sensa ya watu na Makazi Bi Hajjat Amina Mrisho amesema kuwa ili kurahisisha zoezi hilo, anawaomba
wananchi wote wale ambao hawajahesabiwa wapige namba zifuatazo ili waweze
kuhesabiwa,0222122724,0754583415,0222129622,0713335429.
Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria katika mkutano huo wakiwa kazini |