Monday, July 23, 2012

WAZIRI WA MIUNDO MBINU ZANZIBAR AJIUZULU KUTOKANA NA TUKIO LA KUZAMA KWA MELI YA MV SKAGIT

Waziri wa Miundmbinu na Mawasiliano wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (CUF) Hamad Masoud, amejiuzulu wazifa wake  kufuatia ajali ya boti ya MV Skagit, iliyotokea zanzibar hivi karibuni na kusababisha watu kadhaa kupoteza maisha. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la mapinduzi ameridhika kwa kujiuzulu kwa Waziri huyo na tayari amemteua Rashid Seif Selemani (Ziwani CUF) kushika nafasi hiyo. Wakati huohuo Makamu wa pili wa Rais wa Serikali hiyo Balozi Seif Ally Iddi amesema kuwa uamuzi wa kujiuzulu Hamad ni wake binafsi.