Thursday, July 26, 2012

WALIMU KUANZA MGOMO KABLA YA SENSA

Chama cha walimu nchini Tanzania (CWT) Kimeitangazia serikali kuwepo na harufu ya Mgomo ambao imeanza kunukia baada ya  serikali kushindwa kusuluhisha mgogoro wake na walimu.Rais wa Chama cha walimu Gratian Mukoba amesema leo katika makao makuu ya Chama cha walimu jijini Datr es Salaam wakati akiongea na waandishi wa habari kuwa, Tarehe 25 julai saa 4 Asubuhi  CWT  Na serikali zilifika mbele ya Msuluhishi kupewa cheti cha kuonyesha kuwa  Usuluhishi umeshindikana . Ambapo kwa maelezo hayo CWT kiliwaagiza walimu kuanza kupiga kura baada ya kupewa cheti  hicho, ambacho ni kama Kibali cha wao kugoma. Mukoba alisema kuwa zoezi la walimu kupiga kura litaendelea mpaka kesho Asubuhi na baada ya muda huo kupita Chama kitapokea matokeo kutoka kila wilaya na Endapo kura za ndio zitakuwa nyingi mgomo utaanza kabla ya Zoezi la Sensa.
Aidha Mukoba alisema kuwa mgomo wa walimu hauna Mahusiano na zoezi la uesabuji watu (Sensa)  kwa hivyo walimu watashiriki katika sensa kama kawaida na Mgomo utakuwa palepale.