Saturday, July 28, 2012

WALIMU KUANZA KUGOMA JUMATATU,WATABAKI NYUMBANI BILA KWENDA SHULE MPAKA KIELEWEKE


Chama cha walimu kimeitangazia Serikali kuwa Mgomo wake unaanza Rasmi siku ya Jumatatu baada ya kura zilizopigwa na  walimu kuonekana kuwa  asilimia 95.7 ya wanachama  wameunga mkono Mgomo . Raisi wa Chama cha Walimu Tanzania CWT Bw, Gratian Mukoba  amesema leo wakati akiongea na waandishi wa habari kuwa, walimu waliopiga kura ni, Walimu wa shule za awali, Msingi, Sekondari, maafisa waliopo kwenye ukaguzi wa  shule na wakufunzi wa vyuo vya ualimu na maendeleo ya Jamii.
Alisema kuwa  Mgomo huo umeungwa mkono na walimu Takriban 153,848 ambapo ni zaidi ya nusu ya wanachama wote waliopiga kura. Kwa hivyo Baraza la CWT limetoa notisi ya saa 48 kwa serikali  kuanzia jana tarehe 27 julai saa nane mchana na baada ya saa hizo walimu wataanza mgomo wa kubaki nyumbani bila kwenda kazini  kuanzia siku ya   Jumatatu tarehe 30 julai 2012 hadi hapo watakapo arifiwa na Rais wa CWT Bw, Gratian Mukoba.
Mukoba aliwataka walimu kushiriki Mgomo huo ambao ni halali  ambao umeitishwa na chama  kwa mujibu wa Sheria.

Rais wa CWT akionyesha fomu iliyotumwa  kwa maafisa Elimu wa mikoa ili kuorodhesha walimu kwa kuandika Check namba zao, shule wanazofundisha,  na kama wanaunga au hawaungi mkono mgomo huo jambo ambalo Rais amesema kuwa kitendo cha kuwataka walimu wajaze fomu hiyo ni kuwatisha na kuwakatisha tamaa katika jitihada zao za kudai haki zao na.

Rais Mukoba akiongea na waandishi wa habari