Tuesday, July 17, 2012

VIONGOZI WA VYAMA NA SERIKALI WATAKIWA KUTOA USHIRIKIANO KWA MAKARANI WA SENSA

Baadhi ya Wakufuzi wa Sensa waliohudhuria katika ufunguzi wa mafunzo  ya Wakufunzi  wa Sensa  ya Watu na Makazi ya Mwaka 2012 ngazi ya Mkoa wakimsikiliza mgeni Rasmi ambaye alikuwa ni mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mh, Said Meck Sadick.Katika ufunguzi huo Mkuu wa mkoa aliwataka
Viongozi wa Vyama na Serikali katika ngazi zote kwa ujumla  kutoa ushirikiano katika kuhamasisha na kuelimisha umma umuhimu wa kushirikiana na makarani wa sense kwa kutoa taarifa sahihi wakati wa zoezi la kuhesabu watu.
Akihutubia wakati wa kufungua mafunzo ya wakufunzi wa Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2012 Ngazi ya Mkoa wa Dar es Salaam leo, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam  Said Meck Sadiki amewakumbusha wananchi kwamba shughuli zao za kiuchumi na kijamii hazitakwamishwa na zoezi la sense litakalochukua siku zisizozidi saba.
Aidha amewahakikishia wananchi kuwa taarifa zitakazokusanywa zitatumika kwa Siri na zitatumika kwa shughuli za kitakwimu tu, kwa mujibu wa Sheria ya Takwimu ya Mwaka 2002.
 

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadick watatu kutoka kushoto kwa waliokaa akiwa kwenye picha ya Pamoja na Wakufunzi waliohudhuria katika Ufunguzi wa mafunzo hayo.