Wednesday, July 4, 2012

KAMATI YA URITHI WA DUNIA IMEKUBALI OMBI LA KUREKEBISHA MPAKA WA PORI LA AKIBA LA SELOUS

Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe, Khamis Kagasheki (kushoto) akiongea na waandishi wa habari kuhusu
Kamati ya Urithi wa Dunia ya UNESCO katika kikao chake cha 36 kinachoendelea (tarehe 24 June hadi 6 Julai 2012) katika jiji la Saint Petersburg nchini Russia kuwa imelikubali ombi la Tanzania la kuurekebisha mpaka wa Pori la Akiba la Selous, ambalo ni Eneo la Urithi wa Dunia, ili kuruhusu uchimbaji wa Madini ya Urani. Eneo linalohusika ni asilimia 0.8 ya  eneo la Pori la Akiba la Selous. Kagasheki alisema kuwa,
Kwa mara ya kwanza ombi hilo lilipelekwa  kwa Kamati hiyo ya Urithi wa Dunia ya UNESCO mwezi Januari 2011 ambapo lilijadiliwa katika Kikao chake cha 35 ambacho kilihamishia mjadala huo katika  Kikao cha 36 kinachoendelea. Uamuzi huo ulifanyika ili kuruhusu Tathmini ya Athari ya Mazingira (EIA) kukamilishwa na kutoa muda kwa wataalam wa IUCN kufika eneo linalihusika ili kuliona na kuhakiki taarifa ya tathmini hiyo.