Friday, July 27, 2012

IGP WA UGANDA AITAKA TANZANIA KURUDISHA PASSPORT YA CHAMELEON

Mkuu wa jeshi la polisi nchini Uganda,  IGP, Kale Kayihura amewaagiza maofisa wa Tanzania kuirudisha haraka passport ya Jose Chameleone.
Kayihura ametoa amri hiyo alipokutana na Chameleon kwenye kituo cha polisi cha Muyenga mchana wa leo jijini Kampala.
Amesema maafisa wa hapa nchini wamesema passport ya msanii huyo ingewasili baadaye leo na kukabidhiwa kwake mara moja.
Leo Jose Chameleone akiwa na mashabiki wake wameandamana kwenye ubalozi wa Tanzania nchini Uganda kudai arudishiwe passport hiyo iliyokuwa ikishikiliwa na Erick Shigongo kwa madai kuwa meneja wake amemtapeli dola 3500.