
Je hii hali ya kutoamiana kati ya "wagonjwa' na madaktari iliyotengenezwa na serikali itaendelea mpaka lini? Hata wananchi wa kawaida siku hizi huwa hawana imani na tiba wanazopewa hospitalini km kweli ndio best possible ya matibau wanayoweza kupata kutoka kwa madaktari wao! Hii inatokana na kinyongo ambacho bado madaktari wamebaki nacho!
Je serikali inalijua hili na ni nini wanachofanya kuhakikisha watu wa kawaida na viongozi hasa wa CCM wanarudisha imani kwa madaktari wetu? Na ni nini serikali inafanya kuhakikisha wanamaliza kinyongo na manunguniko waliyonayo madaktari ili warudishe moyo wao wa kufanya kazi kwa ufanisi na kujtolea?
Njia ya kutumia nguvu na vyombo vya dola kama mahakama kweli inaweza kurudisha ari, kuaminiana na kujitolea kwa madaktari wetu katikas kuokoa maisha ya watanzania? Tunaomba serikali imalize huu mgogoro na madaktari na washikane mkono na "tuwaone kwenye picha na TV wakicheka" kwa ajili yetu sisi wagonjwa kuturudishia imani hasa na madaktari wetu wa muhimbili ambapo ndipo penye rufaa ya maisha yetu. Imefikia mahali hata ndugu yako akipewa rufaa ya muhimbili roho inakudunda! Tafadhali serikali hebu turudishieni amani ya roho! Tafadhali sana tunaomba sana!