Friday, July 27, 2012

ALIYEPANGA NJAMA ZA KUMUUA MANDELA ANA HATIA

Aliyepanga njama za kutaka kumuuwa rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini, Nelson Mandela amepatikana na hatia baada ya mahakama ya Pretoria kumpata kiongozi kutoka kundi la Boeremag ambapo ilimtaja mtu huyo kuwa ni Bw, Mike Du Toit kuwa alipanga njama za kumuua Mandela Mwaka 2002.
 
Bwana Mike du Toit ndiye aliyepanga milipuko tisa katika eneo la Soweto mjini Johannesburg mwaka 2002.

Kiongozi huyo wa kundi la kibaguzi ni mtu wa kwanza kupatikana na hatia tangu utawala wa viongozi  wengi uanze mwaka 1994 Afrika kusini.

Wachanganuzi wanasema kuwa bado kuna hali ya kutopendana katiki ya watu wa rangi tofauti nchini Afrika kusini.
Hata hivyo kundi kama la Boeremag,inayomaanisha Nguvu za Makaburu miongoni mwa Makaburu ,halina ufuasi mkubwa.
Mahakama hiyo ya Pretoria imempata Du Toit, ambaye alikuwa msomi baada ya kusikiliza kesi hiyo kwa miaka tisa.