Monday, June 11, 2012

WALIMU WATISHIA NYAU SERIKALI; WATOA SIKU 30 TENA KUTATULIWA MATATIZO YAO LA SIVYO....

Raisi wa Chama Cha Walimu Tanzania CWT Bw, Gratian Mukoba (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari juu ya maazimio yao katika baraza la Taifa kuhusu nyongeza ya mishahara na posho ambapo alisema kuwa wanataka matatizo yao kujadiliwa  ikiwemo posho pamoja na nyongeza ya mishahara kwa asilimia mia moja. Aidha Bw, Mukoba alisema kuwa,mabali na kupewa posho pamoja na kuongezewa mishahara pia wanaitaka serikali iwalipe deni lao la kiasi cha sh, Bilioni 13 kwa kukazia hilo Rais huyo alisema kuwa kufikia tarehe sat mwezi wa saba mwaka huu watajua la kuwaambia walimu ikiwa bado hawajapewa jibu la malalamiko yao.

Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria katika mkutano huo wakimsikiliza raisi kwa makini.

Makamu mwenyekiti wa CWT kulia akisistiza jambo katika mkutano huo.