Saturday, June 30, 2012

UJENZI WA KITUO KIPWA CHA POLISI CHAZINDULIWA LEO DAR.

Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mhe Yusuph Mwenda akizungumza na wananchi wa kata ya Sinza leo hii wakati wa Uzinduzi wa ujenzi wa Kituo kipya Cha Polisi,  katika Kata hiyo ambapo Mstahiki Meya huyo aliwataka wananchi wa Eneo hilo kutoa ushirikiano ili ujenzi wa jenngo hilo uweze kukamilika ambapo alisema kuwa zinahitajika zaidi ya milioni hamsini ili jengo hilo liweze kukamilika. Aidha Meya huyo alisema kuwa kwakuhakikisha kuwa ulinzi wa unaimarika maeneo ya Sinza, atahakikisha kuwa Mitaa yote 53 iliyopo Sinza iajengwa vituo vya Polisi. Katika milioni 53 zinazo hitajika kujenga kituo hicho cha polisi tayari Mbunge wa jimbo la Ubungo amechangia Milionio Kumi kutoka kwenye mfuko wa Jimbo.

Msatahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni mhe, Yusuph Mwenda akikata Utepe kuashiria uzinduzi wa ujenzi wa kituo cha Polisi Sinza.

Jiwe la Msingi lililowekwa na Mheshimiwa Meya.

Diwani Kata ya Sinza Mh, Renatus Pamba akiongea na Wananchi wake baada ya uzinduzi wa ujenzi wa kituo hicho ambapo aliwataka wananchi kuhakikisha kuwa wanatoa ushirikiano katika kuhakikisha kuwa Jengo hilo linakamilika na pia aliwataka wananchi wa Sinza kutokujenga katika maeneo ya Serikali ili kuepuka usumbufu wa Kubomolewa kwani mahali kinapojengwa kituo hicho ni mbele ya Nyumba ya mtu ambaye hakutakiwa kujenga katika maeneo hayo.