Saturday, June 16, 2012

KINA MAMA WAPEWA MAFUNZO JUU YA UMUHIMU WA KUJIUNGA NA NHIF

 Mkurugenzi wa Uendeshaji Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya  Nation Health Insurance Fund (NHIF) Bw, Eugen Mkongoti akizungumza na vikundi mbalimbali vya kina mama wapatao (400)  wanaopatiwa elimu juu ya umuhimu na faida za kuwa mwanaschama katika mfuko wa  Bima ya Afya  ambapo alisema kuwa watapata fursa ya kupata matibabu bure kwa watu sita katika familia ambao watakuwa ni Mme na Mke pamoja na watu tegemezi wanne kwa mwanachama mmoja atakayekubali kuwa mwanachama wa NHIF mfuko wa Bima ya Afya mafunzo hayo yanaendelea hivi sasa katika ukumbi ndani ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa DSM.
 Kaimu mkurugenzi wa Bima ya Afya Bw,  Rehani Athmani  akikazia umuhimu wa kinamama kujiunga na kuwa wanaachama katika mfuko huo.
Mkurugenzi Idara ya Uwezeshaji Wanawake (WAMA) Bi, Tabu Likoko akiongea na waandishi wa habari(hawapo pichani) juu ya namna  wanawake watakavyofaidika watakapo amua kuwa wanachama wa mfuko wa Bima ya Afya.
Baadhi ya kinamama walioghudhuria katika mafunzo hayo wakisikiliza kwa makini.