Thursday, June 28, 2012

JOSE CHAMILION KUTUA DAR NA KUFANYA TAMASHA UWANJA WA TAIFA SIKU YA SABASABA

Msanii wa Uganda, Jose Chameleone (kulia) leo amekamilisha taratibu zote za kusaini mkataba wa kufanya shoo kali Uwanja wa Taifa mpya, jijini Dar es salaam, siku ya sabasaba baada ya Meneja Mkuu wa Global Publishers, Abdallah Mrisho, kutia timu Entebe mapema leo. Pichani chini ni Chameleone akijigamba kufanya shoo na akisaini mkataba wa mwisho huku akishuhudiwa na meneja wake. Chameleone ametoa onyo kwa Diamond kuwa atamchakaza na Valuvalu!