Thursday, June 28, 2012

DK ULIMBOKA AMEWEZA KUNYWA MTORI LEO ASUBUHI

Hali ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk. Stephen Ulimboka, inaendelea vizuri katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam alikolazwa jana baada ya kutekwa, kupigwa  na watu wanaodhaniwa kuwa majambazi.

Tetesi tulizozipata kutoka kwa wadau wetu,  kutoka Muhimbili usiku wa kuamkia leo, zimedai kwamba Dk. Ulimboka aliweza kunywa mtori aliopelekewa na madaktari wenzie.


Pia, ilielezwa kuwa waodi aliyolazwa ilikuwa na ulinzi mkali wa madaktari wenzie, ambapo hakuna mtu yeyote asiyefahamika kusogea ama kuingia  kumuona.