Wednesday, June 13, 2012

HII NDIYO BARUA WALIYOANDIKIWA OFISI YA TAKWIMU


                  VIONGOZI WA JUMUIA YA KIISLAMU  
kumb:vjk/01/12

KAMISHNA WA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2012
OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU,
SLP 796
DAR ES SALAAM

YAH: KUTOKUKUBALIANA  NA MSIMAMO WA KIKAO CHA SENSA CHA JUNI 11 MJINI DODOMA       
Husika na Kichwa cha habari hapo juu
Kufuatia kikao kilichoitishwa na Idara ya Takwimu ya Taifa ambacho kiliwahusisha viongozi wa dini  za kikiristo na kiislamu ambacho kilikuwa na Agenda kupokea maoni ya juu mchakato wa sense tunatoa msimamo ufuatao :
1)Waislamu tumesikitishwa sana na msimamo uliotolewa na waziri wa Ofisi ya Rais M ahusiano ya jamii na Uratibu wa kutupilia mabali mapendekezo ya waislamu ya kuingizwa kipengele cha dini  na uwakilishi wa viongozi  wa dini katika tume ya Sensa.
2)Tumesikitishwa na jinsi Waziri Steven Wassira alivyotumia fursa hiyo ya mkutano kuwakejeli viongozi wa kiislamu waliokuwepo kwenye mkutano kwa  kuwaambia kama hamkuelewa somo wenzenu wakristo wameelewa.
3)Kwakuwa matarajio yetu yalikuwa ni kuingiziwa kipengele cha dini kwenye  dodosa za sense, msimamo huo unaendelea kuzingatiwa na jamii ya kiislamu kama kanuni muhimu ya ushiriki wao katika zoezi zima la sensampaka mapendekezo yaliyotajwa hapo juu yazingatiwe.
Tunatanguliza shukrani zetu
Barua hii imetiwa saini na viongozi 31 kutoka jumuia na taasisi mbalimbali za kiislamu walioshiriki semina hii.