Monday, April 16, 2012

MWIZI WA KICHANGA ZANZIBAR AKAMATWA




Jeshi la Polisi Zanzibar linamshikilia mwanamke mmoja mkazi wa Tomondo mjini Zanzibar kwa tuhuma za kuiba mtoto mchanga mwenye umri wa miezi mitano kutoka katika Hospitali Kuu ya Mnazimmoja mjini Zanzibar.
,Na Mohammed Mhina, wa Jeshi la Polisi Zanzibar, amemtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Fatma Abdallah Mohammed(26) ambaye alikamatiwa Bandarini akisafiri na mtoto huyo kwenda Pemba.
 
Kamanda Aziz amesema kuwa mtoto huyo aitwaye Aisha Nassor Ali, aliibwa Aprili 10, mwaka huu majira ya saa tano asubuhi wakati mama wa mtoto huyo  Bi. Rahma Hassan Ali, alipompeleka mtoto wake kupata matibabu katika Hospitali ya Kuu ya Mnazimmoja mjini Zanzibar.
 
Amesema wakati mama wa mtoto huyo akiwa katika foleni ndefu ya kutaka kupata kadi ya kumuona daktari, alitokea mwanamke mwingine ambaye sasa ni mtuhumiwa, akijifanya kuwa ni mwandishi wa Habari na alikuwa akifuatilia kezo za tiba katika Hospitali hiyo, lakini pia alikuwa akifahamiana na mmoja wa madaktari na hivyo kumtaka ampe msaada ili mtoto huyo aweze kupatiwa tiba kwa haraka.
 
Amesema mtuhumiwa huyo aliongea na simu na kujifanya kuwa alikuwa akionge na daktari na bwamba amemtaka apelekwe mtoto huyo kwake kwa matibabu na ndipo mtuhumiwa huyo alipomwambia mama wa mtoto kuwa ampatie mtoto ili atangulie naye kwa daktari na kumtaka mama wa mtoto akatafute daftari la kuandikia matibabu ya mtoto wake.