MAMLAKA
ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), imekamata magari
144 ya abiria kutokana na kufanya makosa mbalimbali.
Akizungumza
na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Ofisa Mfawidhi Kanda
ya Mashariki wa Sumatra, Conrad Shiyo, alisema magari hayo yamekamatwa
kuanzia mwanzoni mwa wiki hii.
Alisema
kati ya magari hayo 63 yaliokamatwa ni kutokana na makosa ya kuwatoza
abiria nauli kinyume na ile elekezi, kutumia tiketi za zamani na
kukatisha njia huku wakijua fika kuwa kufanya hivyo ni kosa.
“Tumegawa
chati za bei kuanzia Jumatatu kwa kila gari, zenye utambuzi wa bei ya
nauli za zamani na mpya hivyo kila mwananchi anayo haki ya kuoneshwa
chati hiyo pindi anapotaka na akinyimwa kuiona hilo ni kosa na mhusika
atachukuliwa hatua,”alisema Shio.
Aliyataja
makosa mengine kuwa ni pamoja na magari 71 ambayo madereva na
makondakta wake walikutwa wakiwa hawakuvaa sare za kazi na matumizi ya
lugha chafu kwa abiria ambako adhabu za makosa hayo faini zake zinaanzia
sh 100,000 na kuendelea.
“Nawashukuru
wananchi kwa ushirikiano wao katika kufanikisha operesheni hii ya
kukamata magari haya, tunawaomba waendelee kutuletea taarifa za madereva
hao ili tuweze kuwashinda wakorofi hawa wasiotaka kutii sheria za
nchi”alisema Shio.
No comments:
Post a Comment