Kaimu
Mganga Mkuu wa Hospitali wa Serikali, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii
Dkt. Donald Mmbando akitoa hotuba ya Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii
Mh. Dk. Hussein Mwinyi wakati wa kufungua rasmi maonyesho ya huduma za
hospitali ya taifa ya Muhimbili katika kuadhimisha miaka 13 ambapo
amezungumzia nia ya serikali kusaidiana na hospitali hiyo katika
kutafutia ufumbuzi changamoto zinazoikabili ili iweze kuendelea kutoa
huduma kwa wananchi katika kiwango cha juu kama ilivyokusudiwa.
Kaimu
Mganga Mkuu wa Hospitali wa Serikali, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii
Dkt. Donald Mmbando (katikati waliokaa)katika picha ya pamoja na wakuu
wa idara mbalimbali na wajumbe wa bodi ya wadhamani mara baada ya
kufungua rasmi maonyesho ya huduma za hospitali ya taifa ya Muhimbili
katika kuadhimisha miaka 13 na miaka mitatu kama hospitali ya ubingwa wa
Juu ya taifa.
*******
Serikali
ya Tanzania imepongezwa kwa juhudi zake ilizofanya na inazoendelea
kufanya kwa sasa katika kuhakikisha kwamba majukumu makubwa matatu ya
Hospitali ya taifa ya Muhimbili yanatekelezwa ipasavyo.
Pongezi
hizo zimetolewa wakati wa ufunguzi wa maonyesho ya huduma za hospitali
ya taifa ya Muhimbili katika kuadhimisha miaka 13 kama hospitali ya
taifa na miaka mitatu kama hospitali ya ubingwa wa juu ya taifa
uliofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Taarifa
ya hospitali hiyo imesema kwa upande wa tiba imefanikiwa kuongeza idadi
ya vitanda kuwa 1271, na kuongeza idara na kuwa 30.
No comments:
Post a Comment