Thursday, April 18, 2013

TCRA yakemea ukiukwaji wa matakwa ya sheria na kanuni za usajili wa namba za simu za mkononi.

 
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Prof. John Nkoma akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa kutoa tamko la pamoja kwa umma la Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania na Makampuni yanayotoa Huduma za Simu kuhusu Usajili wa namba za Simu za Mkononi Tanzania ambapo amesema Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ikishirikiana na makampuni ya Simu na vyombo vya usalama imeanza kampeni endelevu yenye lengo la kuwabaini wote wanaohusika na uvunjifu wa sheria ili kuwalinda watumiaji wema na jamii kwa ujumla kwa ajili ya kuimarisha usalama na kuleta maendeleo na ustawi wa wananchi.
Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya simu za mkononi ya Tigo Tanzania Diego Gutierrez akielezea jinsi kampuni yake ilivyojidhatiti katika kutoa huduma kwa wateja na kuhakikisha kila namba ya simu inayotolewa na kampuni ya simu ya Tigo inasajiliwa kwa mujibu wa kifungu cha 102 (1) cha Sheria ya mawasiliano ya Elektroniki na Posta (EPOCA).


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Prof. John Nkoma (wa tatu kushoto) akiwa meza kuu na Wakurugenzi Watendaji Wakuu wa Kampuni yanayotoa huduma za simu nchini.
Baadhi maafisa mbalimbali na wawakilishi wa makampuni yanayotoa huduma za simu nchini katika mkutano huo.
Sehemu ya wawakilishi mbalimbali wa vyombo vya habari nchini.

No comments:

Post a Comment