Na Mwandishi wetu
Kampuni ya Push Media Mobile imetoa ving’amuzi 91 kwa ajili ya kushindaniwa katika promosheni ya “Kidigitali Zaidi” ambayo lengo lake kubwa ni kuongeza idadi ya watumiaji wa mfumo wa matangaza ya televisheni ya kidigitali.
Meneja Masoko wa Push Media Mobile, Rugambo Rodney (pichani), amesema kuwa promosheni hiyo itaanza kwanza kwa miezi mitatu ambapo kila siku mshindi mmoja atajishindia king’amuzi.
Rugambo alisema kuwa ili kushinda king’amuzi tuma neno “shinda” kwenda namba 15522 na mshindi anaweza kujipatia king’amuzi cha aina ya StarTimes, DiGi Tek au Zuku.
Alisema
kuwa wamesikia kilio cha watanzania kuhusiana na gharama za kupata
king’amuzi na wao kuanzisha promosheni hiyo ambayo washindani watapata
king’amuzi sawa na ‘bure’ na kuzishukuru kampuni za Global Publishers,
Kituo cha televisheni cha DTV, Times FM, Magic FM, Maisha Club na
Baakubwa kwa ushirika wao katika kampeni hiyo.
Kwa
mujibu wa Rugambo, promosheni hiyo ni endelevu na lengo lao ni kuona
watanzania wanapata haki ya kupata habari kwa njia ya televisheni.
“Tumejiandaa
vilivyo kwa ajili ya promosheni hii, kila siku kumekuwa na kilio cha
watanzania kuhusiana na gharama za kupata king’amuzi, wengi hawana na
wanakosa taarifa za kila siku ikiwa pamoja na habari za michezo, sanaa,
urembo na za kisiasa,” alisema Rugambo.
Alisema kuwa jumla ya shs 25 millioni zitatumika katika promosheni
hiyo ambapo mshindi wa siku ya 90 atapata king’amuzi na televisheni
bapa ‘flat screen’ yenye thamani ya sh. 1 million.
No comments:
Post a Comment