Thursday, January 24, 2013

TAASISI YA WAHANDISI WASHAURI TANZANIA (ASET) YAZINDUA OFISI YA KANDA AFRIKA DAR ES SALAAM


Rais wa Shirikisho la Wahandisi la Kimataifa
Ulimwenguni (FIDIC), Geoff French  (kushoto),

akikata
utepe kuashiria ufunguzi wa Ofisi ya
Wahandisi
Washauri
Kanda ya Afrika Tanzania katika hafla

iliyofanyika

Dar es Salaam leo. Kulia ni Rais wa Taasisi ya

Wahandisi Washauri Tanzania (ASET), ambayo

ipo chini ya FIDIC. Mhandisi Menye Manga.

(Picha habari na www.mwaibale.blogspot.com)
Rais wa Shirikisho la Wahandisi la 
Kimataifa

Ulimwenguni (FIDIC), Geoff French  (kulia), akiwa na watendaji wengine wa Taasisi hiyo (wa tatu kulia), ni
Rais wa Taasisi ya Wahandisi Washauri Tanzania (ASET), Mhandisi Menye Manga.

Na Dotto Mwaibale
TAASISI ya Wahandisi Tanzania (ASET), imezindua ofisi za Kanda kwa Bara la Afrika ambayo makao yake makuu ni Dar es Salaam chini ya uongozi wa Watanzania.
Akizindua ofisi hizo Rais wa Kanda ya  utendaji ya shirikisho la kimataifa  la wahandisi washauri (FIDIC), Geoff French, alisema lengo ni kutaka wahandisi wa Tanzania watambulike ndani na nje ya  nchi katika shughuli zake.
“Hii ni ofisi yetu  ya kwanza kufunguliwa katia mikoa mitano Tanzania  ambayo itakuwa inaendeshwa na Mtanzania katika shughuli zake zote pia atashirikiana na viongozi wengine kutoka katika mikoa mingine,”alisema  French.
Alisema wamepanga mikakati mbalimbali katika taasisi hiyo, ikiwemo kutoa mafunzo kwa wahandisi wazawa kutokana na changamoto za teknolojia ambazo zinazoikabili ulimwengu kutokana na idadi ndogo ya wahandisi ambao hawatoshelezi kukidhi mahitaji ya nchi katika kipindi hiki cha sayansi na teknolojia.
Alisema kamati ya utendaji ya Shirikisho la kimataifa  la  wahandisi  washauri
( FIDIC), wameona kuwa ni vyema kuwa na ofisi zake hapa nchini kwani itakuwa ni heshima kubwa kwa Tanzania kutokana na amani iliyopo.

Naye Rais wa  Wahandisi Washauri Tanzania (ACET), Menye Manga, alisema zipo changamoto mbalimbali ambazo zinawakabili katika taasisi hiyo ikiwemo kutojijengea uwezo wa kufanya kazi vizuri pamoja na kutokuwa na wahandisi wa kutosha nchini.

Tumepanga mikakati mbalimbali katika taasisi hii kwa ajili ya kuwaendeleza wahandisi wazawa ikiwemo kuwapa  mafunzo pamoja na kutoa fursa ya wahandisi wengi katika suala la ujuzi wa kazi hii.

“Mafunzo hayo yatatolewa  kwa mhandisi yeyote atakayependa kujiandikisha kwa ajili ya kupata ujuzi zaidi katika kazi yake ambapo mafunzo hayo yatatolewa  kwa muda wa siku mbili. 

“Taasisi yeyote itakayopenda kupata mafunzo hayo wanauwezo wa kuwachukua walimu hao na kuwapa mafunzo hayo kwa muda wa siku tatu au zaidi.
“Ni bora tutoe mafunzo kwa wahandisi kwani kadri siku zinavyoenda wasomi wengi wanapungua kusoma masomo ya sayansi na  hisabati,” alisema Manga.

Alisema  gharama za mafunzo hayo zitapungua au kuongezeka kulingana  na wakufunzi watakaotoa mafunzo hayo kutoka sehemu mbalimbali duniani kama vile Dubai.

Alisema wakufunzi kutoka nje ya nchi watatoa mafunzo hayo kwa gharama ya dola za Marekani 2,000 na wale watakaotoka Tanzania watatoa kwa gharama ya dola za Marekani 850.


Aidha Manga aliwataka wahandisi  waliopo Serikali za Mitaa, Jiji na  Wilaya kujiandikisha katika mafunzo hayo ili waweze kupata elimu ya kutosha juu ya uhandisi.

No comments:

Post a Comment