Wednesday, January 30, 2013

MANISPAA YA ILALA YAFANIKIWA KUZOA TAKA KWA ASILIMIA 50% KWA KIPINDI CHA MWAKA 2005-2012,,.. PIA YAONYESHA MAFANIKIO YAKE KEDEKEDE KATIKA KIPINDI HICHO

Mkuu wa Wilaya ya Ilala
 
Manispaa ya Ilala imefanikiwa kuzoa  50% kati ya  takataka zote  zilizopo katika Manispaa ya Ilala kwa Kipindi cha Mwaka 2005-2012
Hayo yamesemwa Leo na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bw, Raymond Mushi, wakati alipokuwa  akielezea mafanikio ya Serikali ya awamu ya nne  kwa kipindi hicho katika wilaya hiyo.
Mushi amesema kuwa, Kiwango cha uzoaji taka ngumu kimefikia tani 550 kwa siku sawa na tani 198,000 kwa Mwaka ambapo amesema kiwango hicho ni asilimia 50% ya tani 1100 za taka zianazo zalishwa kwa siku.
“Kwa sasa kiwango cha  Uzoaji taka ngumu kinaridhisha kutokana na wilaya kupata vitendea kazi vyenye uwezo Mzuri”, amesema Mkuu wa Wilaya.
Amesema kuwa  Mafanikio hayo, ni Miongoni mwa Mafanikio Mengi ambayo Serikali hiyo imeyafikia kwa kipindi chake tangu imeingia Madarakani na kusema kuwa  wana matumaini kuwa mpaka kufikia mwaka 2015, Manispaa hiyo itakuwa imefanikisha Mengi.
Ameendelea kusema kuwa,  kufanikiwa kwa asilimia hizo kunachangiwa  na kununuliwa kwa Magari sita ya kukandamiza taka yenye Uwezo Mkubwa wa kubeba kati ya tani kumi hadi 24 kwa Safari moja ikiwa ni pamoja na Kununuliwa kwa makasha ya taka 30 na kuwekwa kwenye maeneo yenye uzalishaji Mkubwa wa taka.
Ameendelea kuyataja Mafanikio mengine yaliyopo katika Manispaa hiyo kwa kipindi cha mwaka 2005-2012 kuwa ni, Usambazaji maji ambapo amesema katika Mamlaka ya maji DAWASA imeongeza visima virefu vya Maji kutoka visima 110 mwaka 2005 kufikia 195 na visima vifupi 60 kwa mwaka 2012.
Amesema kuwa, mafanikio hayo yameambatana na Uboreshwaji  wa Huduma za Afya, Ardhi, Kilimo Ujenzi pamoja na Elimu, ambapo Katika Afya Manispaa imefanikiwa kuongeza idadi ya Vituo vya kutolea huduma  kutoka 15 hadi 22 pamoja na Zahanati 20 kutoka 13 zilizokuwepo  kwa mwaka 2005-2012.
Waandishi wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya na kuandika mambo muhimu

“Katika Elimu  zimeongezwa shule za Awali kufikia shule 128 tofauti na ilivyokuwa 2005 ambapo kulikuwa na shule 75 tu, pia Manispaa  imeongeza  madarasa katika shule za msingi pamoja na kuongeza shule za Sekondari ambapo kwa sasa zipo shule  49 zinazomilikiwa na Serikali na shule 42 zisizo za Serikali” amesema.
Hata hivyo katika Sekta ya Ardhi, amesema kuwa jumla ya Viwanja 5,986 vimepimwa kwa matumizi mbalimbali ya Ardhi pamoja na Leseni 28,763 kurasimisha makazi katika maeneo mbalimbali yasiyopimwa,  na amezungumzia pia swala la ujenzi an kusema kuwa kipindi cha 2005-2012 Manispaa imeshuhudia kuwepo kwa Ujenzi mkubwa wa Miundombinu wa Barabara Makaravati, Mifereji ya maji ya Mvua na njia za Watembea kwa Miguu.

Aidha Bw, Mushi amesema kuwa,  Mafanikio Mengine yameonekana katika sekta ya Ajira kwa Vijana,  Kilimo, vyama vya Ushirika, Ajira za Vijana,Shughuli za Kiuchumi na Ujasiria Mali pamoja na Utawala Bora.

No comments:

Post a Comment