Thursday, January 31, 2013

SEMINA KUHUSU MKONGO WA MAWASILIANO YAFANYIKA DAR


 Mkurugenzi Mkuu wa Tehama akifungua semina ya Mkongo wa Mawasiliano iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam na kuwashirikisha wahariri wa vyombo mbalimba vya habari. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni simu Tanzania (TTCL), Said Amir Said na Meneja Uendeshaji wa kampuni hiyo, Adin Mgendi. (Picha na John Dande wa Habari Mseto Blog)   
Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni simu Tanzania (TTCL), Said Amir Said. akifafanua jambo wakati wa semina ya Mkongo wa Mawasiliano iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam na kuwashirikisha wahariri wa vyombo mbalimba vya habari. Kushoto ni Meneja Uendeshaji wa kampuni hiyo, Adin Mgendi. 
 Baadhi ya Wahariri kutoka vyombo mbalimbali vya habari wakiwa katika semina hiyo.
Washiriki wakiwa katika picha ya pamoja.

DAR ES SALAAM, Tanzania

SERIKALI imesema kuwa mradi wa mkongo wa Taifa wa mawasiliano ukisimamiwa na kuendeshwa kwa uaminifu utachangia maendeleo ya nchi ikiwemo kulipa mkopo uliotumika kuujenga.
Mradi huo ambao utapanua soko la mawasiliano kutoka nchi moja hadi tisa.

Akizungumza ijini Dar es Salaam leo wakati wa kufungua semina ya wahariri wa vyombo vya habari Mkurugenzi wa Tehama, Injinia Zaipuna Yonah, alisema kuwa manufaa ya mkongo huo wa mawasiliano yameshaanza kuonekana hasa baada ya kuongezeka ubora na kasi ya matumizi ya mtandao na data pamoja na utoaji wa huduma za elimu mtandao.

Yonah alisema kuwa faida za mkongo zinaonekana na zimekidhi matarajio ya Serikali ya kuziba pengo la matumizi ya Tehama kwa wananchi na kukuza uchumi.

Akizitaja changamoto zilizojitokeza alisema kuwa ni usalama wa miundo mbinu ambayo inapita kwenye makazi ya watu, mashambani, hifadhi za wanyama na kuwataka watanzania kuhakikisha rasilimali niyo inatunzwa.

Pia alisema kuwa Serikali imeikabidhi kampuni ya simu (TTCL) kuhakikisha inasimamia, inaendesha na kuuendeleza mkongo wa mawasiliano ili kuleta mabadiliko ya utendaji na ufanisi wa kazi kupitia Serikali mtandao, elimu mtandao, afya mtandao, kilimo mtandao na kujenga utamaduni mpya wa wanachi kupata taarifaza serikali kwa uwazi.

No comments:

Post a Comment