Saturday, November 17, 2012

JUKWAA LA KATIBA TANZANIA WABAINI MAPUNGUFU YALIYOPO KWENYE MCHAKATO WA KATIBA MPYA

 
JUKWAA LA KATIBA TANZANIA bado tumebaini mapungufu kadhaa katika mchakato wenyewe wa ukusanyaji maoni kwa mwezi huo, ikiwa ni pamoja na Tume kuendelea kutumia huduma ya wataalam wa lugha za alama ili kusaidia watu wenye ulemavu wa kusikia na kuzungumza.
Mikutano kuendelea kufanyika asubuhi na mchana na hivyo kuwanyima fursa ya ushiriki wananchi wengi hususani wanawake.na kucheleweshwa kwa utoaji wa ratiba na hivyo kufanya maandalizi yawe duni katika maeneo wanakojiandaa kwenda.
Kwa ujumla, Tume imeshindwa kushughulikia baadhi ya mapungufu ya Mchakato wa ukusanyaji wa maoni kwa sababu ya kutaka kuwahi kukamilisha mchakato katika tarehe iliyopangwa bila kuzingatia haja ya watanzania wote kutoa maoni yao bila vikwazo.


Inasikitisha kuwa hata ratiba ya mzunguko wa mwisho wa awamu ya kwanza utakaohusisha ukusanyaji maoni katika mikoa ya Dar es Salaam, Mara, Simiyu, Geita, Arusha na Kusini Magharibi ilikuwa haijatoka na kusambazwa hadi Alhamis wiki hii. Ukusanyaji maoni katika Mikoa hiyo unaanza Jumatatu tarehe 19 Novemba na utaendelea hadi 12 December 2012.

No comments:

Post a Comment