Wema naye akionyesha ishara ya kuomba radhi kutokana na Kitendo hicho, na alijitetea kuwa alifanya vile kutokana na kutokuwa na uzoefu wa kucheza jukwaani,"Jukwaa la Fiester lilikuwa ni refu sana na waandishi siku zote wanakaaga kwa chini hivyo ni lazima wangeona kila kitu, hata hivyo napenda kuwahakikishia watanzania kuwa sintorudia na tokea siku ile nimekuwa navaa nguo ndefu kama Jeans ambazo zinasitiri mwili wangu", alisema Wema. Wakati wa kuongea na waandishi wa habari Wema pamoja na Mwenzie walivaa nguo ambazo ni Ndefu za kuwapendeza na ambazo zinasitiri miili yao swali ni Je, Wasanii hawa watabadilika kama walivyo ahidi kubadilika mbele ya Umma? |