Hivi karibuni zilizuka story kuwa Balozi wa Tanzania nchini Malawi amepewa saa 48 awe ameondoka nchini humo lakini imebainika kuwa habari hizo ni za uzushi mtupu na kufwatia uzushi huo Seikali ya malawi imemkamata mwandishi wa habari hiyo kutoka Malawi Justice Mponda(pichani) na amefikishwa mahakamani kwa
kufungua "kiwanda cha kutunga uongo" kuwa Serikali ya Malawi imemwamuru
Balozi wa Tanzania nchini Malawi kuondoka nchini humo ndani ya masaa 48.
Inasemekana mwandishi huyo alikamatwa nyumbani kwake na polisi wenye
silaha mida saa kumi leo alfajiri na kupelekwa kwenye kituo cha polisi
cha Blantyre kwa mahojiano kabla ya kufikishwa mahakamani.
Habari kwa hisani ya Mtandao