Katika Ziara Hiyo Mh Mbunge alifanikiwa kutembelea Makanisa yote yaliyoharibiwa pamoja na kutoa pole kwa Waathirika na kuwataka wawe wavumilivu wakati Dola inafnya kazi yake.
Makamu Askofu wa Kanisa la TAG ambaye kanisa lake lilikumbwa na Vurumashi hiyo alisema kuwa watu walioingia kufanya uharibifu walikuwa wanaharibu pamoja na kupora vitu vingine.
Alisema kuwa katika kanisa lake walikuwa wanavunja vioo vya magari pamoja na Kuchoma Magari lakini kabla ya Kuchoma walikuwa wanaiba baadhi ya vifaa vikiwemo Radio za Magari.
Mh Mbunge (kulia) akiangalia gari liliochomwa katika hekaheka hizo |
Kinanda cha Kanisa la KKT kilichoharibiwa na wahalifu hao |