Baadhi wa wanachama wa chama cha Albino Tanzania waliohudhuria katika hafla ya kukabidhi mafuta hayo |
Mfuko wa Pensheni wa LAPF leo
umetoa msaada wa Lotion za Kuzuia Mionzi ya Jua kwa wanachama wa chama
cha watu wenye ulemavu wa ngozi Dar es Salaam wenye thamani ya zaidi ya
shilingi milioni tano.
LAPF inatambua madhara ya mionzi
ya jua na pia umuhimu wa lotion hizi. inatambua pia mahitaji ni makubwa
zaidi lakini kwa kuanzia imetoa msaada huu wa lotion 140 zenye ujazo wa
100 mls wenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni tano ikiamini kwamba
zitasaidia kupunguza mahitaji hayo. Kadhalika LAPF inawaomba msisite
kuendelea kuwasilisha maombi hayo na itasaidia kadri uwezo utakavyo
ruhusu.
LAPF imekuwa mstari mbele katika
kusaidia makundi mbali mbali yenye ya watu wenye mahitaji maalum katika
jamii hasa watu wenye ulemavu wa ngozi. Kama mtakumbuka mwaka juzi
ilitoa msaada wa shilingi milioni tano kwa ajili ya ujenzi wa boma kwa
Mlemavu wa ngozi aliyekatwa mikono, mwaka jana tulitoa msaada wa fulana
na vifaa mbali mbali kwa chama cha wenye ulemavu wa ngozi Dodoma na
mwaka huu tukaona tuoe msaada huu wa lotion za kulainisha ngozi
Mtambue kuwa LAPF ni Mfuko wa
Pensheni na wanachama wake ni mtu yeyote anaeamua kujiunga na LAPF iwe
ameajiriwa au amejiajiri mwenyewe. Hifadhi ya jamii ni haki ya kila mtu
hivyo tunawashauri ndugu zetu wenye ulemavu wa ngozi mjiunge na Mfuko
huu unaotoa mafao bora zaidi nchini. Kadhalika LAPF imeanzisha mpango
wa akiba wa hiari ambao unamfaa kila mtu na riba yake ni ya ushindani
hivyo mjiwekee akiba kwa faida ya baadae.
Mbali na Mpango huo, LAPF inatoa
Mafao ya Kustaafu, Mafao ya Warithi, Mafao ya Ulemavu, Mafao ya Uzazi na
Msaada wa Mazishi kwa mwanachama aliyefariki. LAPF pia inatoa mikopo ya
Nyumba kwa wanachama wanaokaribia kustaafu pamoja na mikopo ya
wanachama kupitia SACCOS zao. Hivi sasa Mfuko uko kwenye hatua za mwisho
kuanzisha Mafao ya Elimu.