Sunday, October 7, 2012

WACHAKACHUZI WA MBEGU SASA MWISHO WENU UMEFIKA

SERIKALI kupitia wataalamu wake wa kilimo imeanza mkakati wa kutoa elimu ya kisayansi juu ya matumizi ya mbegu za kisasa na madawa kwa wakulima ili kukabiliana na uchakachuaji wa mbegu na madawa unaofanywa na wafanyabiashara wenye tamaa  ya kujiongezea kipato kwa njia ya udanganyifu.
Kauri hiyo imetolewa mwishoni mwa wiki na naibu waziri wa kilimo,Adamu Malima wakati akifungua mkutano wa wataalamu wa mbegu,wakulima,na mawakala wa mbegu kutoka nchini mbalimbali za Afrika uliofanyika jijini Arusha.
Aidha alisema matumizi ya mbegu za mahindi zisizobora yanaifanya Tanzania kupunguza uzalishaji kwa kiasi kikubwa kutokana ukosefu wa mvua za  kutosha ,ambapo  kwa sasa Tanzania inazalisha tani milioni 5 za mahindi pekee huku nchi jirani zikitegemea kununua mazao hapa nchini.
Alisema Tanzania inakabiliwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa mbegu bora zinazoweza kustahimili ukame na kwendana na mabadiliko ya hali ya hewa ,kwani mbegu nyingi zinazotumiwa na wakulima hapa nchini hazina ubora na mara nyingi zinachakachuliwan na mawakala wa mbengu .
‘’tayari mkaguzi wa mbegu ameshaanza kazi ya kupitia upya mawakala wa mbegu na anakwenda vizuri kwahiyo suala la uchakachuaji karibu linafika mwisho’’alisema Malima
Malima alisisitiza kuwa mkakati wa serikali hivi sasa ni kusambaza elimu juu ya matumizi ya sayansi kwenye kuboresha mbegu pamoja na matumizi ya mbolea za kisasa zitakazomwezesha mkulima kuzalisha kiasi kikubwa cha mazao kwa hekari kidogo.
Alisema kuwa wataalamu wetu hapa nchini hawatumiki kama inavyokusudiwa badala yake wamekuwa wakitumiwa na nchi zinazotuzunguka kwa kutoa elimu  na kueleza kwamba serikali imejidhatiti kuhakikisha kuwa wataalamu wake wanasambaza elimu kwa umma ya matumizi ya mbegu bora kama ngano mahindi ,ngano viazi ,mihogo .
Awali mkurugenzi mtendaji wa sekretalieti ya makampuni ya  mbegu hapa nchini (TASTA),Bob Shuma alisema kuwa katika jitihada za kuhakikisha nchi inakuwa na chakula cha kutosha na wakulima wanapata ufanisi wa mbegu  zinazostahimili ukame umeanza.
Alisema lengo la mkutano huo ni kugundua mazao yanayoweza kustahimili ukame na magonjwa ,kubadilishana uzoefu  na utekelezaji wa utafiti wa mbegu mpya zitakazistahilimi ukame ambao  tayari zimeanza kufanyiwa majaribio mkoani Dodoma.
Alisema Mbegu zilizoanza kufanyiwa utekelezaji wa majaribio hapa nchini,chini ya mpango wa mradi wa wema ni mahindi  na pamba.