Monday, October 8, 2012

KIDATO CHA NNE KIKAANGONI LEO

JUMLA ya wanafunzi 481,414 kidato cha nne leo wameanza mitihani ya kukamilisha elimu ya kidato hicho  huku wakijiandaa kuingia kidato cha tano , mtihani ambao utakamilika Oktoba 25 mwaka huu.
Mtihani huo wa kidato cha nne ambao una umuhimu kwa kwa wanafunzi na jamii kwa ujumla, kwani hutumika katika uchaguzi wa watahiniwa wanaotarajiwa kujuiunga na masomo ya kidato cha tano na vyuo mbalimbali.
Aidha, ili watahiniwam na soko la ajira katika taasisis za umma au sekta binafsi ni lazima mhusika awe nacheti cha kidato cha nne.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Tanzania Daima, baadhi ya wanafunzi walisema wanatarajia kufanya mitihani yao kwa mafanikio kwa kuwa wamejiandaa vizuri.
Mmoja wa watahiniwa hao,Sharifa Haroun alisema anamatumaini makubwa ya kufanya vizuri kutokana na kuwa makini katika kipindi chote cha miaka minne ya mafunzo.
Naye Mwantumu Nassoro ambaye ni Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Mloganzila, wilayani Kisarawe mkoa wa Pwani, alisema walimu wamejitahidi hivyo kilichobaki ni kukamilsha kazi iliyoko mbele yao.
Ni hivi karibuni Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo alisema kuhusu usalama wa mitihani, hadi mwishoni mwa wiki mitihani yote ilikuwa salaam, na hakuna mtihani wowote uliyokuwa umevuja katika ngazi yoyote kuanzia Baraza la Mitihani, Mikoa na Halmashauri.
Mulugo aliwakumbusha watahiniwa kuwa, kila mmoja wao anapaswa kufanya mitihani hiyo kwa kujitegemea bila kutumia udanganyifu.
Alitoa onyo kwa wale wote watakaobainika kushiriki katika udanganyifu watachukuliwa hatua za kinidhamu.
Mulugo alitoa witoa wito kuwa walimu, wasimamizi wa mitihani, wakuu wa shule, viongozi wote, na jamii kutoa ushirikiano na kuhakikisha kuwa mitihani inafanyika katika mazingira yenye usalaama na amani.
“Ninaomba wote tuungane kuwaombea watahiniwa wetu baraka za mwenyezi mungu na mafanikio katika mitihani yao”alisema Mulugo.
Akikumbushia walimu waliyojihusisha na vitendo udanganyifu katika mtihani wa mwaka jana, alisema walimu hao walipewa adhabu mbalimbali ikiwemo onyo, karipiokali, kuvuliwa madaraka wakuu wa shule na wengine kushitakiwa TSD.
Aidha, wenye shule binafsi waliothibitika kusababisha udanganyifu wameandikiwa barua ya kusudio la kuzuia kudahili wanafunzi wa kidato cha kwanza kwa muda wa mwaka mmoja.

 Imeandikwa na bukuku blog