Takriban polisi kumi wa Kenya wamejeruhiwa mapema leo asubuhi katika
mlipuko wa guruneti uliotokea wakati polisi walipokuwa wakiendesha msako
katika nyumba moja jijini Mombasa.
Mkuu
wa polisi katika eneo hilo Aggrey Adoli amethibitisha kutokea kwa
mlipuko huo ambao amesema huenda umeendeshwa na watu wenye uhusiano na
wapiganaji wa kundi la Al Shabab.
Hata
hivyo polisi walifaanikiwa kumuuwa mshambuliaji mmoja na mwingine
aliuawa wakati alipojilipua na guruneti. Msakao huo uliendeshwa katika
eneo la Likoni karibu na bandari ya Mombasa baada ya kupewa taarifa za
kuwepo kwa wapiganaji katika eneo hilo. Bunduki mbili, guruneti na
risase vimakamatwa katika msako huo.
Polisi
nchini Kenya imeanzisha operesheni ya kuwasaka wafuasi wa kundi la
Mombasa Republican Concil MRC, kundi ambalo linataka eneo la Mombasa
kujitenga na serikali ya Kenya na kuitewa serikali huru. Watu wawili
waliuawa jumatatu wakati wa operesheni ya kumkamata kiongozi wa kundi
hilo la MRC Omar Mwamunwadzi.
Aggrey Adoli amesema kuwa hakuna uhusiano wowote kati ya operesheni ya leo na kundi la MRC.
Wafuasi
wa kundi la Al Shabab wenye mafungamano na Alqaeda, siku za nyuma
waliendesha mashambulizi dhidi ya polisi wa Kenya katika eneo la
Mombasa, linalo hudhuriwa na watalii wengi kutoka nchi za kigeni na
maeneo mengine ya Kenya pia yalishambuliwa.
---
Taarifa hii ni kwa mujbu wa Ali Bilali, RFI Kiswahili, Mombasa - Kenya