Habari imeandikwa na Woinde Shizza via via blog --
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Magesa Mullongo jana alifanikiwa kuzima jaribio
la mkuu wa shule ya sekondari Peace house iliyopo eneo la Kisongo
jijini Arusha la kumzuia kutofanya mtihani wa kidato cha nne mwanafunzi,
Willbard Moshi aliyekuwa amefukuzwa kwa madai ya utovu wa nidhamu.
Mulongo
alimwamuru mkuu wa shule hiyo Christopher Mushi, kumruhusu mwanafunzi
huyo kufanya mtihani bila masharti yoyote na kumweleza kuwa huo sio
mtihani wa shule hiyo bali ni mtihani wa taifa na ni haki ya msingi kwa
mwanafunzi kuufanya.
Alieleza kuwa
kitendo cha uongozi wa shule yeyote kumzuia mwanafunzi kufanya mtihan
iwa taifa ni kosa kisheria na kwamba mhusika anapaswa kuchukuliwa hatua
kali kwani makosa ya mwanafunzi hayahusiani na mtihani wa taifa na
ukizingatia barua ya kufukuzwa alipatiwa siku moja kabla ya
mtihani, ‘Hairuhusiwi kumsuia mwanafunzi kufanya mtihani labda kama
alifukuzwa muda mrefu haliwezekani lazima mwanafunzi huyo afanye mtihani
kwa hiyo nakuagiza mwalimu mkuu mruhusu mwanafunzi afanye mtihani bila
masharti yoyote’’alisema Mulongo.
Akizungumza
shuleni hapo, Mkuu wa Shule hiyo alidai kuwa mwanafunzi huyo hakupaswa
kufanya mtihani akidai kuwa bodi ya shule hiyo iliridhia kutimuliwa
kwake kutokana na makosa mbalimbali ya utovu wa nidhamu likiwemo la
kukutwa na mwanafunzi wa kike kwenye bweni.
Mkuu
huyo aliongeza kuwa kosa jingine , mwanafunzi huyo aliruka uzio wa
shule na kutoroka katika kipindi cha Sensa hata hivyo alikiri kwamba
uongozi wa shule hiyo haukuwahi kumpatia barua ya onyo ama karipio la
mdomo hadi agosti 7 siku moja kabla ya mtihani wa kidato cha nne,
ilipompatia barua ya kumfukuza shule.
Naye
mlezi wa mwanafunzi huyo, Hadija Juma alipiga kitendo cha mkuu wa shule
hiyo kumzuia mtoto huyo kufanya mtihani akidai kuwa maamuzi hayo
hayakuzingatia sheria na kwamba yalilenga kumkomoa na kupoteza mwelekeo
wa misha ya mwanafunzi huyo.
Alisema
yeye kama mlezi wa mtoto huyo hakuwahi hata siku moja kuitwa na uongozi
wa shule na kufahamisha mwenendo wa mtoto huyo, na siku zote amekuwa
akishirikiana vema na mkuu wa shule hiyo ila alishtushwa sana kupata
barua ya kufukuzwa shule kwa mtoto wake na kuamuriwa kutofanya mtihani
wa kidato cha nne ulionza nchini kote oktoba 8 .
Aliongeza
kuwa baada ya kupata barua hiyo aliamka alfajiri na kwenda shuleni hapo
akiwa na mwanafunzi huyo kwaa lengo la kuonana na mkuu wa shule hiyo,
hata hivyo mkuu huyo alitoa agizo kwa kuwataka walinzi la shule kumzuia
mtu yoyote kuingia ndani ya shule hiyo.
Alisema
kitendo hicho kilimchangaza sana na kuamua kutoa taarifa kwa mwandishi
wa habari hizi ambaye alifika shuleni hapo kwa lengo la kupata taarifa
kamili juu ya kumzuiwa kwa mwanafunzi huyo kufanya mtihani.
Baada
ya maelezo ya mkuu wa shule, mwandishi wa habari hizi aliwaasiliana kwa
njia ya simu na mkuu wa mkoa wa Arusha Magesa Mulongo na baada ya
kuelezwa taarifa hiyo aliamuru kwa kumtaka mkuu wa shule hiyo kumruhusu
mwanafunzi huyo afanye mtihani huo bila masharti yoyote, ambapo
mwanafunzi huyo aliyekuwa tayari amefanikiwa kujipenyeza na kuingia
ndani ya chumba cha mtihani aliendelea kufanya mtihani huo.