Friday, October 12, 2012

KAMANDA KOVA AZUNGUMZIA TUKIO LILILOTOKEA MBAGALA, ASEMA KUWA TUKIO LILIANZA TOKEA JUZI


Kamanda wa Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam ameelezea tukio zima Lililotokea Mbagala na kusema kuwa tukio hilo lilianza juzi octoba 10 ambapo  ambapo kijana mwenye miaka kumi na mbili aliambiwa akikojolea kitabu cha Kuraan utatokewa na nyoka au madhara mengine yatamtokea.

Amesema kuwa Kijana huyo aliamua kukojolea kitabu hicho ndipo kijana huyo wa kiislamu ambao wote walikuwa na utani aliamua kwenda kuwaambia wazazi wake juu ya Tukio zima.
Ndipo wazazi wa huyo kijana wakaamua kukaachini na kuzungumza ili kumaliza kutokana na kuwa  waliofanya hivyo ni watoto

Kamanda Kova amesema kuwa athari zilizotokea mpaka sasa ni kwamba   tayari waislamu hao wamevunja Makanisa  Matatu.
Kamanda ameongeza kuwa hakuna sababu ya kufanya vurugu kwani hayo ni mambo ya watoto kutokana na kuwa mtoto aliyefanya hivyo ni motto wa miaka kumi na mbili.
Naye Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadik amesema kuwa anawaomba wakazi wote wa jiji la Dar es Salaam hasa wale waliopo kwenye eneo la tukio(Mbagala) kuwa wavumilivu ili tatizo hili lililosababishwa na kijana huyo lisiwe chanzo la uvunjifu wa Amani.
Maswala haya tukianza kuleta chokochoko za imani za  kidini mwisho wake huwa unakuwa sio mzuri.