Wednesday, September 26, 2012

MWANDISHI WA HABARI AGNESS YOMO AAGWA LEO JIJINI DAR

Mwili wa aliyekuwa Mwandishi wa Habari wa gazeti la Tanzania Daima, Agness Christopher Yamo umeagwa leo mchana Buguruni, Dar es Salaam, tayari kwa safari ya mazishi kesho mjini Morogoro. Yamo aliyewahi pia kufanya New Habari 2006 Limited, alifariki dunia jana katika hospitali ya Jeshi, Lugalo, Dar es Salaam, alikokuwa amelazwa kwa matibabu.

Katika uagwaji wa mwili wa marehemu, aliyekuwa mcheshi na rafiki wa wengi, mamia walijitokeza na wengi walishindwa kujizuia kiasi cha kulia hadi kupoteza fahamu. Hakika ilikuwa huzuni, simanzi na majonzi eneo la tukio. Agness ameliza watu. Mungu aiweke pema peponi roho ya marehemu, Amin.

hivi ndivyo ilivyokuwa

Huyu ndiye aliyekuwa Mhariri wake mkuu Absalom Kibanda

Mkurugenzi wa Free Media

Baadhi ya waandishi

Buriani mpiganaji