Sunday, September 23, 2012

MBUNGE VITI MAALUMCHADEMA ATOA AHADI YA KUSAIDIA CHANGAMOTO ZILIZOPO KATIKA SHULE YA SEKONDARI MAGNUS

Mbunge wa Viti maalum Chadema Mh, Filipa Mturano akiwa akiuliza swali kuhusu namna ya kuchanganya Kemikali  kutoka kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Magnus ambao walikuwa wanasherehekea Mahafali yao ya Tano leo ambao idadi yao ni wanafunzi 75 wavulana 30 na wasichana 45. Mturano alikuwa Mgeni rasmi katika Mahafali hayo ambapo aliahidi kuwatafutia wafadhili wa kusaidia maendeleo katika  Shule hiyo yenye changamoto ya ukosefu wa  Vitendea kazi katika Chumba cha Computer (Tehama) pamoja na Kukosekana kwa Uzio  inayopelekea wanafunzi wengi kutoroka Shule pamoja na Udogo wa Mabweni hasa kwa Wavulana.
Wanafunzi wa Shule hiyo wakionyesha uwezo wao wa kuchanganya kemikali wakiwa katika Chumba cha Maabara ya Shule hiyo.

Mkuu wa Shule ya Sekondari  Magnus Mwl, Leonce Charles Kayagwa(Kushoto) akitoa maneno machache kabla ya Kumkaribisha Mgeni Rasmi ambapo amezungumzia changamoto mbalimbali katika shule hiyo zikiwemo ukosefu wa kisima cha maji pamoja na wazazi kukosa  muda wa kuwasimamia  watoto wao kusoma nyakati za jioni.

Wahitimu ndio hawa hapa.