Saturday, September 22, 2012

ETI MIONGONI MWA WALE WALIOMZOMEA MIZENGOPINDA WAMEKAMATWA

Kuna taarifa nimezipata kutoka kwa mmoja wa makada wa CCM Mkoani Mwanza kuwa watu 10 wamekamatwa kwa kitendo cha kumzomea Waziri Mkuu Pinda pale uwanja wa Sahara Jijini Mwanza. Kada huyo ya CCM ameonyeshwa kusikitishwa na kitendo hicho akisema kuwa kitendo hicho ni uhuni na kwamba kuzomewa kwa Pinda ni ujumbe unaotakiwa kufanyiwa kazi na CCM na serikali yake na si kukamata watu.

Nimejaribu kuzungumza na baadhi ya askari polisi jijini Mwanza juu ya taarifa hizi, wamekiri kwamba juzi watu sita walikuwa wamekamatwa na polisi kitengo cha intelijensia kwa mahojiano kuhusiana na Pinda kuzomewa hata hivyo wamesema hawajui kama waliendelea kushikiliwa au waliachiwa. Aidha nimezungumza na mmoja wa askari wa kitengo hicho yeye amekanusha vikali habari hizi.


Tufuatilie ili tujue ukweli kisha tujadiri kama ni halali kumkamata mtu eti kisa kamzomea kiongozi wa serikali kwa kusema hatuitaki CCM! Source Jamii Forum