Thursday, October 30, 2014

WATOTO WA KIAFRIKA WAPEWA KIPIGO BAADA YA KUITWA EBOLA

Big Boys From Senegal_optWatoto wawili wa kiume wenye umri wa miaka 11 na 13 wameshushiwa makonde wanafunzi wenzao na kuwaita jina la ‘Ebola’.
Watoto hao wawili raia wa Senegal walihamia Marekani mwezi mmoja uliopita ‘waliporomoshewa kipigo’ wakiwa shuleni I.S 318, New York katika viwanja vya michezo ambapo wenzao waligoma kushiriki nao michezo na kwa kile walichodai wataambukizwa Ebola na baadaye kuwazonga na kuwapiga.
Taarifa zinasema baba wa watoto hao, Ousame Drame amekuwa akipewa taarifa na watoto wake kuwa tangu wafike shuleni hapo wamekuwa wakinyanyapaliwa kwa kuitwa Ebola, kitu ambacho kimekuwa kikiwakasirisha na kumtaka baba yao awarudishe Senegal.
Idara ya Elimu New York imethibitisha kupokea taarifa zinazohusu vijana hao.
Baba huyo amesema japo watoto hao wamekulia Senegal lakini wana haki za kuishi Marekani kwa kuwa walizaliwa huko, na moja ya matatizo linalowakabili ni kutokujua lugha ya kiingereza kutokana na kukulia nchini Senegal ambako inazungumzwa lugha ya Kifaransa.

No comments:

Post a Comment