Friday, September 19, 2014

HIVI NDIVYO WAANDISHI WA HABARI WALIVYOPIGWA NA POLISI JANA JIJINI DAR


Mwandishi wa habari Badi akilia baada ya kushambuliwa na Polisi,huyu ni moja ya waandishi walioshambuliwa

Kuna taarifa kuwa mwaandishi wa habari wa IPP Media kapigwa na jeshi la polisi alipokuwa ameenda kuripoti matukio yaliyokuwa yanaendelea baada ya mwenyekiti wa CHADEMA Mhe, Mbowe alipoenda kuitikia wito wa jeshi hilo la polisi.
Habari zinasema kuwa baada ya Mbowe na wanasheria kuingia ndani polisi walianza kupiga kila aliyekuwa eneo la tukio bila kujali ni nani ndipo alipojikuta mwandishi huyo akipigwa mpaka kupoteza fahamu...(MC)
Imeelezwa kuwa waandishi wengi wa habari wameumia vibaya kutokana na kukimbizwa na mbwa wa polisi huku wengine wakiumwa na mbwa hao.
Waandishi wa habari wameshindwa kutimiza wajibu wao kwa kuzuiwa na polisi ambao wameshindwa kutambua uwepo wa waandishi wa habari,Je Uhuru wa vyombo vya habari uko wapi Tanzania? na kama waandishi wa habari wameanza kuumizwa mapemaa kabisa kabla hata kampeni za uchaguzi hazijaanza,Sijui uchaguzi ukifika hali itakuwaje!!
Ikumbukwe kuwa Mwaka jana mwandishi wa habari Daud Mwangosi aliuawa kikatili kwa amri ya RPC (Kamuhanda) wa Iringa wa wakati huo ambaye baada ya kutimiza azima yake hiyo alipandishwa cheo.
Mami ya watu leo wamejitokeza kumsindikiza Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, baada ya kuhitajiwa kufika Makao Makuu ya Jeshi la Polisi nchini, jijini Dar es Salaam kuhusiana na kauli yake aliyotoa Septemba 14 mwaka huu,juu ya kuitisha maandamano nchi nzima kupinga kuendelea kwa Bunge Maalum la Katiba.
Kilichofuata ni polisi kuamuru watu wote waondoke eneo hilo kwa umbali wa mita 200 ambapo walikimbizwa na mbwa wa polisi na kusababisha wengi wao waumie na kupoteza vitu vyao mbalimbali, hususani wanahabari ambao baadhi yao waliumia na kupoteza zana zao za kazi.
CHANZO; GPL

No comments:

Post a Comment