Friday, July 11, 2014

KUHUSU BENKI KUU KUTANGAZA KUTENGENEZA SARAFU YA SHILINGI MIA TANO HUU NDO UKWELI

Screen Shot 2014-07-11 at 9.42.15 AMBaada ya kuripotiwa kuwepo kwa mabadiliko ya noti ya sh. 500 ambayo itaacha kutumika siku chache zijazo nchini Tanzania na mbadala wake kuwa sarafu ya shilingi 500, Watanzania mbalimbali wamekuwa na wasiwasi na taarifa hiyo pamoja pia na kuamini uchumi wa nchi unaanguka.
millardayo.com imepata nafasi ya kuongea na mchumi wa benki kuu kwenye kurugenzi ya utafiti na sera za uchumi Lusajo Mwankemwa ambae amejibu hizo headlines kwa kusema hiki kifuatacho.

‘Kwa niaba ya benki kuu ya Tanzania amewatoa hofu kuhusu haya mabadiliko na kusema haijaja kutokana na ukuaji na ushukaji wa uchumi wa nchi ya Tanzania, yaani kuanza kutumika kwa hii sarafu hakuhusiani na Tanzania kushuka kiuchumi’

Screen Shot 2014-07-11 at 9.44.35 AM‘Noti ya 500 imeonekana inachakaa sana ndani ya miezi 6 kutokana na kuwa na mzunguko mkubwa ikilinganishwa na noti nyingine na haipitii ule mfumo wa kawaida wa kibenki kurudi benki kuu kwa ajili ya kuibadilisha, tulitarajia Mwananchi anapokwenda bank kupeleka pesa zake basi na 500 iwe miongioni mwa hizo pesa ili tuzibadilishe kwa kutoa noti mpya ambazo tunazo benki kuu lakini haijawa hivyo’
‘Tumegundua Mwananchi anaitumia ile mia tano huku chini ambapo pesa anazopeleka benki ni shilingi elfu mbili, elfu 5 na elfu 10 lakini 500 anabakiza kwenye droo kwa ajili ya matumizi madogomadogo, matokeo yake inatumika huku chini kwenye mikono ya watu na haipati kurudi kwenye mfumo wa kibenki kubadilishwa ndio maana tumeona ni busara kuiondoa na kuleta sarafu’
‘Kiuchumi hili halina muingiliano wa moja kwa moja, itambulike kwamba kinachofanywa ni kuondoa noti ya 500 yenye thamani ya 500 na kuleta sarafu yenye thamani ileile ya shilingi 500, kwahiyo thamani iko palepale’

No comments:

Post a Comment