Saturday, July 26, 2014

FUATILIA HABARI KALI 10 ZA LEO JULY 24/2014 KWENYE MITANDAO YA KIJAMII:RAY ASHINDWA KUMZIKA BABA YAKE JOHARI

MKURUGENZI wa RJ Company, Vincent Kigosi ‘Ray’ ameshindwa kumzika baba mdogo wa mkurugenzi mwenza wa kampuni hiyo, Blandina Chagula, Clement Kiyenze Chagula.

Mkurugenzi wa RJ Company, Vincent Kigosi ‘Ray’
Mzee huyo alifariki katika Hospitali ya Muhimbili kutokana na matatizo ya presha na figo yaliyokuwa yakimsumbua na kuzikwa katika Makaburi ya Kinondoni jijini Dar ambapo wasanii mbalimbali wa filamu nchini walishiriki akiwemo Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete.
 Mkurugenzi mwenza wa kampuni hiyo, Blandina Chagula akiwa msibani.
Alipoulizwa Ray kwa nini hakuhudhuria mazishi hayo, alisema:
“Ukweli ni kwamba mimi sipo Dar. Ndiyo maana sijaonekana huko kwenye mazishi, nipo Mwanza katika shughuli zangu za kikazi, tuko pamoja lakini,” alisema Ray.

No comments:

Post a Comment